Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto),
akimkabidhi kadi ya CCM, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Wilaya ya
Nachingwea na Kaimu Mwenyekiti wa Umoja wa Akina Mama wa Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilayani humo, Manufreda Mathias
Malenga. Kiongozi huyo pamoja na wanachama wengine 22 wa chama hicho
wamekikimbia chama chao na kujiunga na CCM na kufanyiwa sherehe kubwa
iliyofanyika katika Kata ya Mtua ambayo Waziri Chikawe alikuwa mgeni
rasmi, aliwapokea wanachama hao na kuwapa kadi pamoja na sare za CCM ili
kuanza mapambano ya kupambana na upinzani Wilayani humo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea,
Mathias Chikawe, akimpongeza Mwenyekiti wa Vijana wa Chadema Kata ya
Mtua, Habibu Oswadi (kushoto), baada ya kukabidhi kadi ya chama chake.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea,
Mathias Chikawe, akizungumza na Viongozi wa CCM Wilaya, Kata pamoja na
wananchi waliofurika katika Uwanja uliopo jirani na Ofisi za CCM Kata ya
Mtua katika sherehe kubwa ya kuwapokea viongozi wawili na wanachama 21
wa Chadema waliojiunga na CCM Wilayani humo. Waziri Chikawe alikuwa
mgeni rasmi, ambapo aliwapokea wanachama hao na kuwapa kadi pamoja na
sare za CCM ili kuanza mapambano ya kupambana na upinzani wilayani humo.
Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo.
Mwanachama
mpya wa CCM ambaye alikuwa Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Wilaya ya
Nachingwea na Kaimu Mwenyekiti wa Umoja wa Akina Mama wa Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani Nachingwea, Manufreda Mathias
Malenga akizungumza kwa hisia baada ya kupewa nafasi kueleza furaha
yake baada ya kukabidhi kadi ya Chadema na kupewa kadi pamoja na sare za
CCM. Malenga aliwashukuru Viongozi na wanachama wa CCM kwa kumkaribisha
katika chama hicho na kuahidi kutoa ushirikiano wake ndani ya chama
hicho. Kiongozi huyo pamoja na wanachama wengine 22 wa chama hicho
wamekikimbia chama chao na kujiunga na CCM na kufanyiwa sherehe kubwa
iliyofanyika katika Kata ya Mtua ambayo Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe
(katikati meza kuu), alikuwa mgeni rasmi aliwapokea wanachama hao na
kuwapa kadi pamoja na sare za CCM ili kuanza mapambano ya kupambana na
upinzani wilayani humo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea,
Mathias Chikawe (watano kulia waliosimama), akiwa na wanachama wapya wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya kukikimbia chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA). Wananchama hao 23 wakiongozwa na aliyekuwa Mjumbe
wa Kamati Tendaji ya Wilaya ya Nachingwea na Kaimu Mwenyekiti wa Umoja
wa Akina Mama wa chama hicho Wilayani Nachingwea, Manufreda Malenga
(watano kushoto waliosimama), walifanyiwa sherehe kubwa iliyofanyika
katika Kata ya Mtua ambayo Waziri Chikawe alikuwa mgeni rasmi aliwapokea
wanachama hao na kuwapa kadi pamoja na sare za CCM ili kuanza mapambano
ya kupambana na upinzani wilayani humo.
No comments:
Post a Comment