Mtalaam wa Mawasiliano wa Tigo, Amani Nkurlu (kulia), akikabidhi tuzo
ya 'Tigo Best Short Film', kwa Mtayarishaji wa Filamu kutoka Kenya Mark
Maina, katika Maonesho ya Filamu ya Kiafrika Arusha (AAFF), aliyeshinda kupitia filamu yake mpya iitwayo "Consigned to
Oblivion." Maonesho hayo yaliyodhaminiwa na Tigo yalifikia tamati juzi.
Mratibu wa maonesho ya AAFF, Nassir Mohamed, akionyesha tuzo aliyoipokea
kwa niaba ya Muongozaji filamu kutoka Tanzania, Amil Shivji, aliyeshinda
tuzo ya 'Best Short Film', kwa ukanda wa Afrika Mashariki kupitia filamu
yake mpya iitwayo "Samaki Mchangani." Akishuhudia kulia ni Mtalaam wa
Mawasiliano wa Tigo, Amani Nkurlu.
Wacheza filamu kutoka nchi za Afrika Mashariki (Burundi, Rwanda, Uganda,
Kenya, Tanzania na Zanzibar), wakionesha vyeti vyao vya kuhitimu mafunzo
maalum ya uchezaji na uandaaji wa filamu kutoka kwa magwiji mbali mbali wa
uandaaji wa filamu barani Afrika.
Wageni waalikwa mbali mbali na wapenzi wa filamu wakipata burudani
kutoka kundi la Reggae kutoka Tanzania, Kenya na Marekani 'The Warriors
from the East' wakitoa burudani.
No comments:
Post a Comment