Jeshi la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatoa taarifa kwa wananchi wote kuwa ni
kosa kisheria kumiliki au kuvaa sare za JWTZ kwa mtu yeyote asiyehusika.
Aidha, kumeonekana
matukio kadhaa ya baadhi ya vikundi, ama mtu mmoja mmoja kumiliki au
kuvaa sare za JWTZ.
Inakumbushwa kuwa, kwa yeyote atakayeonekana amevaa
ama kumiliki sare hizo sheria itachukua mkondo wake.
Imetolewa na:
Kurugenzi wa Habari na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
No comments:
Post a Comment