Mkuu
wa Wilaya ya Uvinza, Mwalimu Hadijah Nyembo (kulia), akitoa nasaha zake
kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali
Mstaafu Issa Machibya (wa pili kulia), kuzungumza na wakazi wa Wilaya ya
Uvinza, kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo cha Redio jamii Uvinza FM
mkoani Kigoma. Kutoka kushoto ni Meneja wa Huduma za Kijamii wa Airtel
Tanzania, Hawa Bayumi, Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa
Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), ambao ndio wadhamini
wakuu wa Redio Uvinza FM, Bi. Rose Haji, Mwalimu na Mkurugenzi Mtendaji
wa Uvinza FM Redio, Bi. Nuru Kalufya.
Na Mwandishi wetu, Uvinza – Kigoma
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya amesisitiza
uadilifu katika vyombo vya habari jamii kwa kutangaza habari zisizoumiza
hisia kwa wananchi wengine na kuepuka migogoro.
Akizindua
kituo cha redio jamii cha Uvinza FM, Luteni Kanali Mstaafu Machibya
alisema kuwa vyombo vina wakati mgumu hasa katika kipindi cha kuelekea
uchaguzi mkuu mwaka 2015.
“Changamoto hii inaweza kuepukika kwa kuhakikisha habari zinazotolewa
zinalenga kuendeleza utamaduni wa amani, upendo, utulivu na uvumilivu na
kuepuka viashiria vinavyoweza kusambaza chuki kwa lengo la kufanikisha
chaguzi salama.
Mkuu
wa Mkoa huyo amesisitiza umuhimu wa kuutumia uhuru wa kutoa na kupata
habari vizuri kwa kusema kwamba uhuru huo usitumike kutoa habari
zinazopendelea upande mmoja na kukandamiza mwingine kwa kuwa hali kama
hiyo husababisha machafuko.
“Kwa
mujibu wa Ibara ya 18 (b) ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania
ya mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari
bila ya kujali mipaka ya nchi, lakini haki hiyo iende sambamba kwa
kuzingatia Sheria za nchi na kuhakikisha habari hizo haziumizi hisia za
wananchi wengine,”
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya, akisoma risala
wakati wa uzinduzi wa kituo cha Redio Jamii, Uvinza FM, ambapo
alilipongeza shirika la UNESCO kwa juhudi na kuwaweka karibu wananchi na
serikali kupitia mawasiliano ya redio.
Luteni
Kanali Mstaafu Issa Machibya, ameitaka redio jamii Uvinza kuonyesha
uwezo wao ili waweze kujitangaza na kujijengea imani kwa wanajamii wao
kuwa wanaweza.
“Ni kwa hali hiyo tu mtaweza kujulikana, kutambulika na
kupata udhamini na matangazo ya kutosha.”
Amewataka
wanajamii kukitumia vyema kituo chao cha redio ili kiwe chachu ya
kuleta na kukuza maendeleo katika vijiji, wilaya, mkoa na taifa kwa
ujumla.
Wakati
huo huo Mkuu wa Mkoa ameitaka redio jamii ya Uvinza kutangaza habari
zenye kuonyesha madhara ya mila potofu na kujenga uelewa wa jamii kuhusu
mila hizo hususan mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino),
kufichua wagonjwa wanaohofia kuwa na dalili za ugonjwa wa ebola na
uharibifu wa mazingira.
Amelipongeza
shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO) kwa kutoa msaada wa vifaa vya kituo hicho na
kuendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wanahabari jamii, Kampuni ya simu
za mkononi ya Airtel kwa kuruhusu matangazo ya Uvinza FM Redio yarushwe
kupitia mnara wake na waanzilishi wa kituo hicho.
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya, akikata utepe
kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM, chini ya
ufadhili wa Shirika la UNESCO na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel
Tanzania. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Meneja wa Huduma za Kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mwalikishi wa Shirika la
Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), ambaye pia ni Mshauri
na Mkufunzi wa redio jamii, Bi Rose Haji Mwalimu, pamoja na Mkurugenzi
Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya, akifanyiwa
mahojiano mafupi ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM na Mtangazaji
wa kituo hicho, Kadisilaus Simon, mara baada ya kuzindua rasmi redio
hiyo.
No comments:
Post a Comment