KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 29, 2015

HOJA YA LIPUMBA YAJADILIWA BUNGENI NA KAULI YA 'WAPIGWE TU YAJIRUDIA'

Spika wa Bunge, Anna Makinda akifafanua jambo bungeni 
 Bunge la Jamhuri ya Muungano leo limejadili kitendo cha uvunjifu wa amani uliotokea kwenye maandamano ya CUF yaliyoongozwa na Profesa Ibrahimu Lipumba jijini Dar es Salaam
Katika mjadala huo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mathias Chikawe aliomba suala hilo kupewa muda wa kufanyiwa uchunguza yakinifu na vyombo husika, wakati Mwanasheria Mkuu George Masaju akitaka suala hilo lisijadiliwe bungeni kwa kuwa tayari limeshafikishwa Mahakamani.
Kabla ya mjadala huo Waziri Chikawe alisoma taarifa yake ya kile kilichotokea kwenye vurugu hizo huku akieleza kuwa taarifa za uchunguzi wa ndani ndizo zililishawishi jeshi la Polisi kuwaomba Cuf kutofanya maandamano yao.
Waziri Chikawe amelieleza Bunge kuwa baada ya taarifa za polisi kutolewa wafuasi wa Chama hicho hawakutaka kutii amri hiyo, hivyo ili kunusuru uvunjifu mkubwa wa Amani ambao ungeweza kutokea walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi hao wa CUF waliokuwepo.
“Nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa sheria na kanuni, haitakuwa busara kila mtu kujifanyia mambo yake anayotaka bila kuzingatia sheria, nimeagiza vyombo husika kuchunguza suala hili, na ikibainika kuwa polisi walitumia nguvu kubwa watawajibishwa kwa mujibu wa sheria. Amesema Chikawe.
Baada ya kauli hiyo ndipo Mwanasheria Mkuu wa Serikali alipolieleza bunge kuwa tayari kesi hiyo imeshafikishwa mahakamani, hivyo kujadili suala hilo bungeni ni kukiuka sheria ya mgawanyo wa madaraka katika mihimili ya dola,jambo ambalo lilipingwa na idadi kubwa ya wabunge.MWANANCHI

No comments:

Post a Comment