![]() |
| Spika wa Bunge, Anna Makinda akifafanua jambo bungeni |
Katika mjadala huo Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi Mathias Chikawe aliomba suala hilo kupewa muda wa kufanyiwa
uchunguza yakinifu na vyombo husika, wakati Mwanasheria Mkuu George
Masaju akitaka suala hilo lisijadiliwe bungeni kwa kuwa tayari
limeshafikishwa Mahakamani.
Kabla ya mjadala huo Waziri Chikawe alisoma
taarifa yake ya kile kilichotokea kwenye vurugu hizo huku akieleza kuwa
taarifa za uchunguzi wa ndani ndizo zililishawishi jeshi la Polisi
kuwaomba Cuf kutofanya maandamano yao.
Waziri Chikawe amelieleza Bunge kuwa baada ya
taarifa za polisi kutolewa wafuasi wa Chama hicho hawakutaka kutii amri
hiyo, hivyo ili kunusuru uvunjifu mkubwa wa Amani ambao ungeweza kutokea
walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi hao wa CUF waliokuwepo.
“Nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa sheria na
kanuni, haitakuwa busara kila mtu kujifanyia mambo yake anayotaka bila
kuzingatia sheria, nimeagiza vyombo husika kuchunguza suala hili, na
ikibainika kuwa polisi walitumia nguvu kubwa watawajibishwa kwa mujibu
wa sheria. Amesema Chikawe.
Baada ya kauli hiyo ndipo Mwanasheria Mkuu wa
Serikali alipolieleza bunge kuwa tayari kesi hiyo imeshafikishwa
mahakamani, hivyo kujadili suala hilo bungeni ni kukiuka sheria ya
mgawanyo wa madaraka katika mihimili ya dola,jambo ambalo lilipingwa na
idadi kubwa ya wabunge.MWANANCHI



No comments:
Post a Comment