Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya Kifaru Abdallah
Mwomboke iliyopo katika wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro akiwa anatoa
neno lake la shukrani kwa Benki ya CBA kwa kufika na kuguswa kusaidia
hosteli ya wasichana katika shule hiyo kutokana na wengi wameshindwa
kuendelea na masomo shuleni baada ya kuingizwa katika mahusiano na
wanaume hali ambayo inawawia vingumu kuweza kumudu masomo.
|
Meneja masoko wa Benki ya CBA Tanzania Solomon Kawishe akizungumza na wanafunzi(hawapo pichani) kuhusu nia yao ya kuwasaidia msaada huo wa saruji kwaajili ya kujenga hosteli ni kutokana na idadi ya wanafunzi 944 kuwa na changamoto kubwa ya ufaulu hasa jinsia ya kike huku akiwaasa wanafunzi hao kuwa Elimu ndio urithi pekee wa kuweza kuharakisha maendeleo Tanzania hivyo jamii inategemea kupata watu muhimu wakuwasaidia kama madaktari,wafanyakazi wa mabenki na hata walimu wa kuendeleza elimu |
No comments:
Post a Comment