Lucas Kadawi Limbu akisisitiza jambo |
Anayejiita Mwenyekiti wa ACT-Tanzania,
Lucas Kadawi Limbu (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi
wa habari Dar es Salaam jana, ambapo alipinga Msajili wa Vyama Siasa
Nchini, Jaji Francis Mtungi kubadilisha jina la chama cha ACT-Tanzania
na kuwa ACT-Wazalendo bila ya kufuata utaratibu. Kulia ni Katibu Muenezi
wa chama hicho, Fredy Kisena na Katibu Mkuu wa chama hicho, Leopold
Mahona.
Na Dotto Mwaibale
Anayejiita Mwenyekiti
wa Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania), Lucas
Kadawi Limbu amemlalamkia Msaji wa Vyama vya Siasa Nchini, Jaji Mstaafu
Francis Mtungi kwa madai ya kukiuka utaratibu wa kubadilisha jina la
chama hicho na kuwa ACT-Wazalendo.
Limbu alitoa malalamiko hayo mbele za waandishi wa habari Dar es Salaam jana na kuhoji nyuma ya ACT-Wazalendo kuna nini.
“Tunashangazwa
na jaji Mtungi kwa kubadili jina la chama chetu bila ya kufuata
taratibu huku akijua fika kuna kesi ya msingi ipo mahakama kuhusu
mwenendo wa chama hicho. Alisema Limbu
Aliongeza kuwa kuna njama za
makusudi zilizofanywa za kubadilisha jina la chama hicho kwani haiwezeka
na haiingii akilini kubadilisha jina la chama kwa kipindi kifupi na
haraka kiasi hicho.
“ACT-Tanzania ni chama chetu sio
cha Zitto na kama anahitahi siasa safi aanzishe chama chake kwani
nafasi hiyo ipo wazi kwa kila mtanzania.
Alisema ni jambo la ajabu kuona
chama kinafanya mkutano wake mkuu wenye nia hofu na kumpatia mtu
madaraka ya kioongozi mkuu na kubadilisha jina lake huku msajili wa
vyama akishuhudia.
Alisema msajili wa vyama vya
siasa alitoa tamko la kubadilishwa jina la chama hicho tarehe 20-4-2015
wakati tayari kiongozi mkuu wa chama hicho kilichobadilishwa jina akiwa
katika zaira ya kichama mikoani aliyoianza tarehe 10-4-2015 huku
wakigawa kadi kwa kupitia chama cha ATC-Wazalendo.
Limbu alihoji fedha zinazotumika
kwenye ziara hiyo na za kuchapa kadi, bendera za chama na vifaa vingine
kuwa zinatoka wapi kama hakuna watu wenye nia mbaya na chama cha
ATC-Tanzania.
(Imeandaliwa na mtandao wa http://www.habarizajamii.com/)
|
No comments:
Post a Comment