KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 24, 2015

KIONGOZI WA UPINZANI BURUNDI AUAWA

Kiongozi wa chama kidogo cha upinzani nchini Burundi ameuawa kwa kupigwa risasi.
Mwili wa Zedi Feruzi pamoja na wa mlinzi wake ulipatikana nje ya nyumba yake kwenye mji mkuu Bujumbura.
Mauaji ya mwanasiasa huyo yanafanyika wakati wanaharakati wa upinzani nchini humo wamesitisha kwa siku mbili maandamano yao dhidi ya rais Pierre Nkurunziza kupinga uamuzi wake wa kuwania urais muhula wa tatu.
Uamuzi huo ambao wengine wanasema kuwa unaenda kinyume na sheria umesababisha kuwepo kwa jaribio la kumpindua,maandamano ya wiki kadha na kuhama kwa zaidi ya watu 100,000 kutoka nchini humo.BBC

No comments:

Post a Comment