Bunge
la Madagascar limepiga kura kumuondoa Rais madarakani hatua ambayo
itarudisha nyuma nchi hiyo iliyokubwa na machafuko miaka iliyopia.
Hatua ya kumuondoa Rais Hery
Rajaonarimampianina iliungwa mkono na wa Bunge 121 kati ya wabunge 125
ambao walipiga kura jana.Uamuzi huo ni lazima uthibitishwe na mahakama
ya katiba.
Rais
Rajaonarimampianina aliingia madarakani Januari 2014 baada baada ya
uchaguzi wa kidemokrasia tangu 2006. Ilitarajiwa kuwa uchaguzi huo
ungemaliza mzozo wa kisiasa nchini humo baada ya mtangulizi wake Marc
Ravalomanana kuondolewa kwenye mapinduzi ya mwaka 2009.
Lakini wapinzani wa Rais wanasema ameshindwa kutekeleza majukumu yake na hivyo hana budi kutoka.
Marekani,
awali ilikuwa ikimuunga mkono Rais huyo, mwaka jana Marekani iliondoa
vikwazo kwa nchi hiyo baada ya kufanya uchaguzi wa kidemokrasia
|
May 28, 2015
WABUNGE WA MADASCAR WAPIGA KURA KUMUONDOA RAIS
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment