KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 23, 2015

MAGUFULI KIMYAKIMYA.

Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, ambaye ni miongoni mwa mawaziri 13 waliochukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), jana alirejesha fomu hiyo kimya kimya huku akikwepa kuzungumzia safari yake ya kusaka wadhamini katika mikoa 23 aliyopita.
 
Magufuli aliyechukua fomu hiyo Juni 5, mwaka huu, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, zikiwa ni siku mbili tangu chama hicho kifungue milango kwa wagombea urais kuchukua fomu.
 
Hata hivyo, Dk. Magufuli, hakuwahi kutangaza nia wala kuzungumza na Watanzania kupitia vyombo vya habari kama walivyofanya makada wenzake waliojitosa kutaka kumrithi Rais Jakaya Kikwete.
 
Tangu alipotangaza nia, Dk. Magufuli hajawahi kueleza vipaumbele vyake iwapo atateuliwa na chama chake kugombea kiti hicho, wala kujinasibu kama wagombea wenzake wanavyofanya kila mkoa waliopita kusaka wadhamini na kisha kupewa fursa ya kuzungumza na wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla. Akiwa Makao Makuu ya CCM mjini hapa, Waziri Magufuli alikabidhi fomu yake kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rajab Luhwavi, saa 4:10 asubuhi ikiwa na wadhamini 450 pekee.
 
Akikabidhi fomu hiyo, Waziri Magufuli alisema: “Nimezunguka katika mikoa 23 ya nchi hii na nimepata wadhamini kwenye mikoa 15, kikanuni inapaswa kuwa hivyo lakini nina ziada ya wadhamini kutoka mikoa ya Tabora, Geita, Mwanza, Kilimanjaro, Mtwara, Mara, Iringa, Pemba na Unguja. Mkitaka niwakabidhi pia kuonyesha ninavyokubalika nitawapa,” alisema na kuongeza: “Mheshimiwa huko kote nilikokwenda nilikuwa natumia ramani ambayo inaonyesha nimepita wapi na wapi? Nimekuja nayo naomba nikukabidhi Mheshimiwa Naibu Katibu Mkuu Bara.” Alipomaliza aligoma kuzungumza na vyombo vya habari na kuondoka. 
 

No comments:

Post a Comment