KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

July 31, 2015

KOCHA MZUNGU ATUA MAJIMAJI

Kocha mpya wa Majimaji kutoka Finland, Mika
Kocha mpya wa Majimaji kutoka Finland, Mika Lonnstorm (Kulia) akiwa na mwenyeji wake, Makamu Mwenyekiti wa Majimaji, John Nchimbi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere juzi. 

Dar es Salaam. Klabu ya Majimaji ya Songea imejiunga na klabu nyingine za Ligi Kuu kuajiri kocha kutoka nje ya Afrika.
Klabu hiyo imemwajiri kocha kutoka Finland, Mika Lonnstrom aliyetua nchini juzi usiku na kuahidi kuifanyia makubwa timu hiyo maarufu, Wanalizombe.
Mika (41) ambaye alipokewa na mwenyeji wake, Makamu Mwenyekiti wa Majimaji, John Nchimbi alipelekwa katika Hoteli ya Sea Cliff.
Gharama za kulala katika hoteli hiyo ya kitalii ni Dola 250 (Sh500,000) kwa siku. Kocha huyo ataishi hotelini hapo kwa siku tatu, sawa na Sh1.5 milioni na leo alitarajiwa kwenda Songea, Ruvuma kwa ndege tayari kuanza maandalizi yake ya msimu mpya wa Ligi Kuu.
Majimaji inayodhaminiwa na Kampuni Symbion, imesaini mkataba wa mwaka moja na kocha huyo mwenye vyeti vya Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa), leseni A.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mika ambaye uongozi umemtambulisha kama mkurugenzi wa benchi la ufundi, lakini ipo wazi ndiye atakayekuwa kocha mkuu, alisema: “Nimekuja Majimaji kwa lengo la kuifanya iwe timu ya ushindani.
“Nimefuatilia na kugundua kuwa ilikuwa timu kubwa na maarufu hapo zamani, lakini ikashuka, mimi nataka kuirudisha kwenye heshima yake.”
Kwa upande wa Nchimbi, alisema: “Tumeamua kumleta Mika kwa ajili ya kuboresha timu yetu, yeye ni mgeni amefundisha timu mbalimbali na maelezo yake binafsi yameonyesha ni mzuri kiufundi na ataisaidia timu yetu.”
Aliongeza: “Pia imekuwa kawaida kwa wachezaji wetu, wanapokuwa na kocha wa kigeni, nidhamu inakuwa juu tofauti na wanapofundishwa na kocha mzawa.”
Aliyekuwa kocha wa klabu hiyo, Hassan Banyai ataendelea na ajira yake ya ukocha kama kawaida.
Mika amewahi kufundisha soka Wales, Finland na Thailand akiwa na klabu za Roi Eti United FC, Gulf Saraburi FC na Police United FC, zote za Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment