Komredi Mugabe |
Habari za uamuuzi wa Mahakama kuhusu ndoa ya
jinsia moja ,zimefika Zimbabwe,ambako Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe alinukuliwa
na redio ya taifa akisema hajafurahishwa na hukumu hiyo na jinsi Rais
Obama anavyounga mkono ndoa hizo ,
“Ndo nimeipata taarifa hii –tangu Rais Obama kukubali ndoa za jinsia moja ,na kuruhusu
watu wa jinsia moja,kutetea ,kufurahia muonekano –hivyo
kama itakuwa lazima, nitasafiri Washington, DC, nitapiga
magoti na kuomba kumshika mkono wake.
Kama huongei lugha ya Mugabe, anasema Mugabe kwamba Rais
Obama kukubali ndoa ya jinsia moja ina maanisha kuwa na yeye labla ni shoga
na kutania kuwa anataka kumuoa ,Mugabe anasema utani huo unalenga katika kuonyesha kuwa ndoa za jinsia
moja ni upumbavu , Mwanamume kumtongoza mwanamume mwenzie ni wendawazimu .
Mugabe amekuwa mpinzani wa ndoa za jinsia moja kwa
miaka mingi,ni njia yake ya kutafuta umaarufu
na kukwepa mambo ya msingi anatumia ndoa ya jinsia moja kumpinga Rais Obama
ambaye ni maarufu Afrika.
"Sasa tunaye huyu Rais Obama , amezaliwa na
baba mwafrika ambaye anasema kuwa hatatoa misaada ikiwa hamtakumbatia ushoga ," Mugabe alisema mwaka 2013. "tunauliza,
alizaliwa kupitia ushoga?tunataka kuendeleza Uafrika, na hiyo inatoka kwa
mwanamke na siyo kwa ushoga John na John, hapana ; Maria na Maria hapana”
Upinzani dhidi
ya ushoga unaendeshwa na watu wanaopenda umaarufu kama Mugabe, ni tatizo kwa nchi za kusini mwa jangwa
la sahara ambako wanachukulia ushoga
kuwa na kosa la jinai .Utafiti unaonyesha kuwa jamii nyingi za nchi za
Afrika hazikubaliani na ushoga
Wakati haki za mashoga zikiboreka katika maeneo mengi ,hali ni mbaya Kusini mwa Jangwa la Sahara . Ripoti ya mwaka 2013 ya shirika la haki za
binaadamu la Umoja wa Mataifa inasema hali ni mbaya Afrika
Kwanini ni kwa Obama? Utawala wa Obama umekuwa
ukiuunga mkono ndoa za jinsia moja Afrika jambo ambalo limekumbana na upinzani
wa viongozi wanao tafuta umarufu kama Mugabe . KWA HISANI YA THE MAIL
No comments:
Post a Comment