Staa wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’
amefunguka kuwa kutoonekana kwake kwenye ushabiki wa vyama na wagombea kama
wasanii wengine si kwamba hana ushabiki lakini moyoni mwake yupo Team ya Dk.
John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kajala aliliambia Ijumaa Wikienda
kuwa pamoja na mbwembwe za watu kujiweka wazi kuhusu chama na wagombea
wanaowakubali, yeye mambo yake ni kimyakimya kama alivyo mgombea wake wa urais
kupitia chama hicho.
“Nimekuwa kimya kwa muda mrefu kwa sababu hata mgombea
wangu wa urais, Magufuli ni mtu wa kimyakimya ila mtendaji mzuri, ndiye
anastahili kura yangu,” alisema Kajala.
Global Publishers
|
August 31, 2015
KAJALA; MIMI NI TEAM MAGUFULI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment