Kinyanganyiro
cha shindano la kukata na shoka la dansi 100% ambalo limekuwa
likiendelea kwa kushirikisha makundi mbalimbali vya sanaa chini ya
uandalizi
wa kituo cha EATV na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania linafikia
kileleni hapo kesho ambapo makundi matano(5) yatachuana vikali katika
kombe pamoja na kitita cha shilingi milioni tano(5) ziotakazokabidhiwa
na wadhamini wakuu wa shindano hilo.
Makundi ambayo yatawasha moto kwenye uwanja wa Don Bosco Oysterbay hapo kesho ni
Team Makorokocho, Best boys kaka zao,The winners Crew,Team ya Shamba na The W.D.
Akiongea
kuhusiana na fainali hizo Mratibu wa shindano hili, Happy Shame alisema
kuwa maandalizi kwa ajili ya mchuano huo yamekamilika na fainali
zitakuwa
na mchuano mkali kwa kuwa makundi yote yanayoshiriki ni mazuri na
yamejiandaa ipasavyo na kundi litakaloibuka kidedea na ushindi
litajinyakulia kitita cha shilingi milioni 5 kutoka Vodacom Tanzania.
“Tunatarajia
fainali zitakuwa na msisimko mkubwa kuwa wasanii wanaoshiriki ni wazuri
na tunafurahi mwaka hadi mwaka ubora wa shindano hili unaongezeka
na kuwavutia watu wengi wakiwemo wapenzi wa muziki wa dansi
nchini,Alisema shame.
Kwa
upande wake Matina Nkurlu, Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania ambao
ni wadhamini wakuu wa shindano hili alitoa wito kwa wasanii wa muziki wa
kizazi
kipya kujitokeza kwa wingi katika fainali hizo kuwaunga mkono madansa
hao na kuchagua kundi moja wapo ili waweze kufanya nao kazi siku za
usoni.
“Shindano
hili haliwahusu madansa na vijana peke yake bali watu wote wakiwemo
mapromota wanakaribishwa kuja kushuhudia na kuweza kuwashika mkono
vijana
hawa ili waweze kujituma zaidi katika kazi yao hii ya kudansi
wanayoitolea jasho ikiwa ni moja ya ajira kubwa kwa vijana wetu”alisema
Nkurlu.
Alisema
kuwa sanaa ikitiliwa mkazo na kufanyika kwa umakini itawawezesha vijana
wengi kujiajiri na kujipatia mapato ya kuwawezesha kuendesha maisha yao
vizuri “Vodacom
tayari tunatambua kuwa sanaa na michezo inaweza kuinua hali ya maisha
ya vijana kwa kupunguza tatizo la ajira ndio maana kampuni imejikita
kudhamini mashindano mbalimbali ya sanaa ikiwemo shindano hili la Dansi
100% na daima tutaendelea kuwa mstari wa mbele
kuunga mkono jitihada za serikali za kupambana na tatizo la ajira kwa
vijana.
Mratibu wa shindano la Dance 100% Happy Shame(kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)kuhusiana na jinsi walivyojipanga kwa fainali ya shindano hilo litakalofanyika kesho katika Viwanja vya Don Bosco Upanga jijini Dar es Salaam ambapo kundi litakaloshinda litaondoka na kitita cha shilingi Milioni tano toka kwa wadhamini wakuu wa shindano hilo Vodacom Tanzania,Shindano hilo limeandaliwa na EATV. |
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa kutangaza fainali za shindano la Dance 100% litakalofanyika kesho katika Viwanja vya Don Bosco Upanga jijini Dar es Salaam ambapo kundi litakaloshinda litaondoka na kitita cha shilingi Milioni tano toka kwa wadhamini wakuu wa shindano hilo Vodacom Tanzania,Shindano hilo limeandaliwa na EATV. |
Alisema
ushahidi upo wa vijana wengi hapa nchini ambao miaka michache iliyopita
hawakuwa na maisha ya uhakika lakini
hivi sasa wanaendesha maisha yao vizuri kutokana na kazi za sanaa
wanazozifanya baadhi yao wakiwa ni wanamuziki na wengine wachezaji wa
michezo mbalimbali.
“Baadhi
ya sanaa na michezo kama vile kucheza dansi,kuimba nyimbo,kucheza mpira
wa miguu,kucheza tenesi,kucheza mpira
wa mikono,riadha,mpira wa pete,bila kusahau tasnia ya filamu ambayo
wasanii wengi waTanzania wamekuwa na mwamko nayo hivi sasa ni ajira
tosha kwa vijana ikifanywa kwa umakini na wadau kuwawezesha washiriki na
serikali inaweza kupata mapato kupitia fani hizi”Alisema
Nkurlu.
No comments:
Post a Comment