KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 7, 2016

JK AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MAALUM MJINI DODOMA

  Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akimsalimia Mumbe wa Kamati Kuu, Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa,  baada ya kuwasili ukumbini kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM leo, Chamwino mkoani Dodoma
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais Dk. John Magufuli akimsalimia Mjumbe wa Kamati Kuu mwenzake, Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Maaliwa
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsalimia Mumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais Dk. John Magufuli kabla ya kikao kuanza. Katikati yao ni Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
 Viongozi hao wakiendelea na mazungumzo ya hapa na pale kabla ya kikao kuanza
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo, kulia ni Mjumbe wa Kamati Kuu Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk John Pombe Magufuli na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Wajumbe wakisimama ukumbini kumlaki Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kabla ya kikao kuanza
 Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais Dk John Magufuli na Makamu wake, Mama Samia Suluhu Hassan wakiwa ukumbini
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye akibadilishana mawazo na Katibu wa NEC anayeshughulikia mambo ya Nje Dk. Asha-Rose Migiro ukumbini. Kulia ni Katibu wa NEC Oganaizesheni Mohammed Seif Khatib
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajabu Luhavi akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ally Vuai na Balozi Seif Ali Idd  ukumbini
 Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Pindi Chana na Asha Aboud wakibadilishana mawazo ukumbini 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa utangulizi kumkaribisha Mwenyekiti kufungua kikao
Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiendesha kikao cha Kamati Kuu Maalum ya CCM, leo, Ikulu Ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment