Ratiba ya michuano ya Kombe la
Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) imetolewa leo, ambapo jumla ya
timu 16 zinakutana katika hatua hiyo (16 bora) itakayoanza kutimua vumbi
wikiendi ya Februari 26-1 Machi 2015 katika viwanja mbalimbali nchini.
Michuano hiyo iliyoshirikisha
jumla ya timu 64 kutoka ngazi za Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi
Daraja la Pili, inaingia katika mzunguko wa nne huku kukiwa na timu
kutoka katika ngazi zote za ligi za TFF nchini.
Ijumaa tarehe 26 Februari
kutachezwa michezo miwili ambapo, Ndanda FC watawakaribisha JKT Ruvu
katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, huku Coastal Union
wakiwa wenyeji wa wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga.
Jumamosi, Februari 27, Mwadui FC
watawakaribisha Rhino Rangers katika uwanja wa Mwadui Complex –
Shinyanga, Jijini Mbeya Tanzania Prisons watacheza na mshindi kati ya
Mbeya City/Wenda FC kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Februari 28, michezo mitatu
itachezwa, Simba SC watawakaribisha Singida United katika uwanja wa
Taifa jijini Dar es salaam, Panone FC watacheza dhidi ya Azam FC uwanja
wa Ushirika mjini Moshi, huku Toto African wakicheza na wachimba madini
wa Geita Gold katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Raundi hiyo itamalizika Machi 01,
2015 kwa mchezo mmoja kuchezwa ambapo Young Africans watawakaribisha
JKT Mlale katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Bingwa wa michuano ya Kombe la
Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mwaka huu ataiwakilisha Tanzania
kwenye Mashindano ya kombe la Shirikisho Barani Africa (CAF CC) mwakani
2017.
No comments:
Post a Comment