Mkufunzi wa Manchester United Louis
Van Gaal amesema kuwa atakata tamaa iwapo Manchester United ilifanya
mazungumzo na Jose Mourinho.
United haikutoa tamko lolote baada ya
ripoti hizo za juma lililopita kwamba maafisa wa kilabu hiyo walifanya
mazungumzo na wawakilishi wa aliyekuwa mkufunzi wa Chelsea Jose
Mourinho.Alipoulizwa iwapo anafikiri kulikuwa na mazungumzo,Van Gaal alisema: katika soka hilo linawezekana,lakini sidhani kama kulikuwa na mazungumzo. Amesema kuwa alikuwa na uhusiano mzuri na mkurugenzi mkuu wa United Ed Woodward na mmiliki Glazers na kwamba wangemwambia. Manchester United kwa sasa hawako katika michuano ya kilabu bingwa Ulaya,na wako nafasi ya tano katika jedwali la ligi ikiwa pointi sita nyuma ya manchester City ambao wako katika nafasi ya nne. |
February 13, 2016
MAWASILIANO NA MOURINHO YATANIKATISHA TAMAA-VAN GAAL
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment