Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akiongozana na Mwanamuziki Diamond Plutnamz pamoja na
Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti Clods FM Bw. Ruge Mutahaba wakati wa
matembezi ya mshikamano kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa kampeni ya usafi
wa jiji la Dar es salaam itakayofanyika kwa siku 90 ikishirikisha
wenyeviti wa mitaa, wananchi katika maeneo yao, Taasisi za Serikali na
Mashirika Binafsi ili kuhakikisha jiji la Dar es salaam linakuwa safi
kabisa.
Makonda amewaambia wananchi mara
baada ya matembezi hayo kwamba Dar es salaam bila uchafu inawezekana na
amenzisha shindano kwa wenyeviti wa mitaa iliyopangwa na isiyopangwa
mwenyekiti atakayeshinda kwa usafi katika eneo lake atajishindia
shilingi milini 50.000.000 na mwenyekiti atakayekuwa wa mwisho katika
eneo lake atapata nafasi ya kutangazwa katika vyombo mbalimbali vya
habari kuhusiana na uchafu uliopo katika eneo lake na wananchi wake na
pia mazingira hayo machafu yataonyeshwa yakiambatana na picha za
mwenyekiti huyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Raymond Mushi
na Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti Radio Clods Bw. Ruge Mutahaba na
Mwanamitindo Millen Magesse ambaye pia ameshiriki kikamilifu katika
kampeni hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Raymond Mushi
na Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti Radio Clods Bw. Ruge Mutahaba na
Mwanamitindo Millen Magesse ambaye pia ameshiriki kikamilifu katika
kampeni hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akiongozana na Diamond Plutnamz huku ulinzi ukiwa
umeimarishwa wakati wa matembezi hayo yaliyofanyika leo kwa ajili ya
kuhamasisha wakazi wa jiji la Dar es salaam kufanya usafi katika maeneo
yao.Haya
ni miongozi mwa matukio yaliyojiri wakati wa matembezi hayo ya
kuhamashiwa wakazi wa jiji kufanya usaifi ambapo kampeni maalum ya siku
90 za kufanya usafi zimezinduliwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda.
Wapiga picha waliendelea na
ubunifu wa kutafuta picha nzuri kama wanavyoonekana hapa kwenye picha
wakiwa kwenye pikipiki wakipiga picha katika matembezi hayo.
Baadhi ya washiriki wa matembezi
hayo wakifanya mazoezi mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Leaders
jijini Dar es salaam ambako ndiko kampeni hiyo ilikozinduliwa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akishiriki katika mazoezi hayo mara baada ya mtembezi hayo
kuwasili katika viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akisalimiana na viongozi wa dini waliofika katika uzinduzi
wa kampeni hiyo ambao ni Sheikh Mkuu wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Mussa Salim na Askofu David Mwasota kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi
No comments:
Post a Comment