KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 21, 2016

ZOEZI LA UOKOAJI WA MIILI YA WALIOZAMA LAKAMILIKA

fe1
Waokoaji wakiwa wamebeba moja ya miili ya watu waliokufa kwa maji mara baada ya gari aina ya Hiace walilokuwemo katika Kivuko cha MV Kigamboni kuopolewa kutoka baharini.

fe2
Moja ya Magari ya Kikosi cha zimamoto likiwa katika eneo la tukio wakati wa uokoaji huo.
………………………………………………………………………………….

Zoezi la uokoaji Gari aina ya Toyota Hiace lililozama baharini leo tarehe 20/04/2015 saa 10 alfajiri, likiwa na watu wawili, limekamilika saa 12:00 jioni hii, baada ya miili  hiyo kutolewa kwenye maji na gari hilo kupatikana.

Gari hilo lililokuwa kwenye MV. Kigamboni kutokea upande wa Magogoni kuelekea upande Kigamboni, likiwa imeegeshwa ndani ya kivuko, ghafla lilitoka kwenye kivuko na kuzama baharini likiwa na dereva mmoja na abiria mmoja.

Shughuli za uvushaji abiria magari na mizigo siku ya leo zimeendelea kwa vivuko vyote viwili
TEMESA inapenda kutoa wito kwa watumiaji wa vivuko vyote kuzingatia maelekezo yanayotolewa na mabaharia wanaofanya kazi kwenye vivuko hivyo.

Uongozi wa TEMESA unatoa pole kwa ndugu na jamaa wa marehemu walio poteza maisha.
Aidha uongozi wa TEMESA unatoa shukrani kwa wale wote waliofanikisha zoezi la ukoaji wakiwemo; Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji, Kikosicha Jeshi la Wanamaji, Mamlaka ya Bandari, Polisi Kikosi cha Maji pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali waliofika eneo la tukio

No comments:

Post a Comment