Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Emmanuel Humba, (kulia), akimkaribisha Naibu Waziri wa Kazi Mhe. Anthony Mavunde alipowasilili kufungua mafunzo kwa Madaktari
yanayohusu ajali na maginjwa yanayosababishwa na kazi Jijini Arusha Leo. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba
…………………………………………………………………………………………
Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), umeendelea na kampeni
yake ya kutoa mafunzo kwa madaktari ili kujenga uelewa wa kufanya
tathmini ya ajali na magonjwa ayapatayo mfanyakazi yanayotokana na kazi
safari hii ikihusisha madaktari kutoka mikoa mitano ya ambayo ni Arusha
Tanga, Manyara, Kilimanjaro na Singida.
Mafunzo hayo yaliyofunguliwa leo
Mei 30, 2016 na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,
Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Bw. Anthony Mavunde, huko
jijini Arusha, ni muendelezo wa mafunzo mengine kama hayo yaliyotolewa
wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, ambapo madaktari kutoka
mikoa ya Dares Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma, lindi na mtwara walihudhuria.
WCF imechukua hatua hiyo ili kujiandaa na UTOAJI WA Mafao kwa mara ya kwanza tangu uanzishwe ifikapo Julai mwaka huu wa 2016.
|
May 30, 2016
MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI, WCF WAENDELEA NA KAMPENI YA KUELIMISHA MADAKTARI KUHUSU FIDIA KWA WAFANYAKAZI WAPATAPO MADHARA KATIKA KAZI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment