KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 27, 2016

JAMII IMESHAURIWA KUBADILISHA MFUMO WA KUKAA NJE YA NYUMBA ZAO KUEPUKA KUPATA MAAMBUKIZO YA UGONJWA WA MALARIA

PEMBA-ZANZIBAR
Na  Masanja Mabula –Pemba
———————————-
JAMII imeshauriwa kubadilisha mfumo wa kupenda kukaa nje ya nyumba zao kwa ajili ya mazungumzo hasa nyakati za usiku ili kuepuka kupata maambukizo ya ugonjwa wa malaria .
Mkuu wa kitengo cha kudhibiti ugonjwa wa malaria Pemba Bakar Omar Khatib alitoa ushauri huo wakati akizungumza na maafisa wa Wizara ya afya kutoka Wilaya ya Micheweni na Wete kwenye  mkutano wa uhamasishaji zoezi la utoaji wa vyandarua  vilivyotiwa dawa uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha uwalimu Benjamini Mkapa.
Amesema kwamba utafiti uliofanywa na wataalamu wa kitengo hicho umebaini kwamba  mbu anayesababisha malaria hupenda kukaa nje ya nyumba na kwamba  njia ya kukabiliana na ugonjwa huo ni kwa jamii kuachana na tabia ya kukaa nje kufanya mazungumzo .
“Mbu anayesababisha malaria nao ni wajanja wanapenda kukaa nje , hivyo ili kukabioliana na ugonjwa huu , ni vyema jamii kubadilisha mfumo wa kukaa ya nje ya nyumba zao kwa ajili ya mazungumzo ”alifahamisha.
Aidha amesema kwamba kutokana na hali hiyo , walio katika hatari   ya kupata maambulizi ya ugonjwa huo  zaidi ni watu wazima kuliko watoto kwani ndiyo wanaopenda kukaa nje , hususani kwa  kuangalia TV na mazungumzo .
Nao washiriki wa kikioa hicho wamekishauri kitengo hicho kuzungumza na makampuni ya simu za mikononi ili yatumike kusambaza ujumbe ka wamiliki wa simu unaotambulisha matumizi sahihi ya vyandarua .
Juma Shaame Salim kutoka mamlaka ya usimamizi wa mazingira Wilaya ya Wete , alisema utaratibu huo utasaidia kufikisha ujumbe kwa wananchi kwa wakati muafaka kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanamiliki ya simu za mikononi
“Kutokana umuhimu wa suala hili ,  ni vyema kitengo hichi kuzungumza na makampuni wa simu za mikononi ili yasaidie kueneza ujumbe kwani wananchi wengi wanamiliki simu za mikononi ”alishauri .
Naye Ali Rajabu kutoka Wilaya ya Micheweni akichangia kaatika mkutano huo aliomba kitengo kuandaa sheria ndogo ndogo ambazo zitatumika akuwabana wananchi ambao wanavitumia vyandarua kinyume na ilivyokusudiwa
Alifahamisha kwamba baadhi ya maeneo ya wilaya hiyo vyandarua vimezungushiwa bustani huku baadhi wakivitumia kwa ajili ya uvuvi wa dagaa , jambo ambalo  linakwamisha ufanisi wamapambano dhidin ya malaria .
Akifunga kikao hicho kwa niaba ya Afisa Mdhamini wizara ya afya pemba , dk Harouk Khalifan hamad alisema mapambano dhidi ya malaria yanahitaji nguvu ya pamoja kutoka wadau na wananchi wote .
katika zoezi la ugawaji wa vyandarua kwa msimu huu jumla ya wananchi laki mbili hasini na tisa elfu na mia nane thelethini na sita (259,836) ambapo walioandikishwa ni wananchi laki nne sitini na saba elfu nan mia saba na sitini na tatu (467,763) kwa kisiwa cha Pemba .

No comments:

Post a Comment