Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi
ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (katikati)
akisalimiana na mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi
(TPSF), Dk. Reginald Mengi (kulia) alipowasili katika ofisi za ESRF
jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini, Mh. Malika
Berak.
(Picha na Modewjiblog)
Taasisi ya utoaji mafunzo ya
Ufaransa ya AFPA ndiyo ilikuwa inaendesha mafunzo hayo wakibadilishana
uzoefu na wadau wa Tanzania kutoka sekta binafsi.
Akifafanua zaidi Dkt. Kida
alisema kwamba kongamano hilo limelenga zaidi katika kubadilishana
uzoefu kuhusu changamoto zinazojitokeza na fursa zilizopo katika
mafunzo, ukuzaji na uendelezaji taaluma.
Dkt. Kida alifurahishwa na
mchanganyiko wa watu kutoka sekta binafsi waliofika katika kongamano
hilo ambao aliamini kwamba wataelezea uzoefu wao katika kukabiliana na
changamoto za taaluma katika makampuni yao.
Aidha alisema kwamba wadau hao
wa Tanzania watapata uzoefu wa timu ya wataalamu wanne kutoka kwa wakala
wa mafunzo ya taaluma nchini Ufaransa (AFPA) ambao wataeleza miaka 60
ya uzoefu katika masuala ya mafunzo ya taaluma na uendelezaji wa
utaalamu.
|
Balozi wa
Ufaransa nchini, Mh. Malika Berak (kushoto) akibadilishana mawazo na
mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald
Mengi (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa
Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida katika ofisi za ESRF jijini
Dar es Salaam.
Alisema anaamini kwamba
mchanganyiko huo wa wadau utasaidia katika kukabiliana na tatizo la
taaluma katika soko la ajira la Tanzania.
Alisema mazungumzo hayo ni
muhimu sana katika kuibua fursa hasa wakati taifa hili linajipanga
kuelekea katika uchumi wa kati wa viwanda na bila wataalamu wenye
taaluma zao makamapuni na viwanda vingi vitakuwa na shida kubwa.
Alisema changamoto kubwa
inayokabili taifa la Tanzania kuelekea nchi ya viwanda kama ilivyo
katika nchi nyingine zinazoendelea ni ukosefu wa taaluma na utaalamu.
“Ukosefu wa wafanyakazi wenye
taaluma katika ngazi zote ni tatizo kubwa linalokabili harakati za
kuelekea uchumi wa viwanda” alisema Dkt. Kida.
Anasema pamoja na matatizo hayo
taasisi yake tayari imeshaanza kushughulikia shida hiyo ya taaluma
nchini Tanzania kwa kuwa na makongamano mbalimbali makubwa
yanayokutanisha wadau kuzungumzia hali hiyo.
|
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi
ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kulia)
akiongozana na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)
Dkt. Tonia Kandiero kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano wa ESRF. Nyuma ni
Balozi wa Ufaransa nchini, Mh. Malika Berak akibadilishana mawazo na
mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald
Mengi pamoja na Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu, Ally Msaki.
Naye Balozi wa Ufaransa nchini,
Mh. Malika Berack amesema kwamba kuwapo kwa taasisi hiyo ya Ufaransa
kushea elimu na watanzania kutasaidia kuinua na kuboresha fursa za
maendeleo hasa rasilimali watu katika utaalamu.
Alisema AFPA yenye uwezo wa
miaka mingi katika kuendesha mafunzo ana tumaini itasaidia kuamsha
ushindani na kuziba mapengo ya wafanyakazi wataalamu katika nafasi
mbalimbali.
Aidha alitoa wito wa kuwapo kwa
sera ambapo Tanzania na Ufaransa zitashirikiana kuhakikisha kwamba
kunakuwapo na mwendelezo katika suala la utaalamu na taaluma kwani hiyo
ndiyo inayoweza kusaidia kusukuma mbele maendeleo ya viwanda.
Alisema AFPA yenye wataalamu
zaidi ya elfu 80 wakiwa wamebobea katika uandazi wa watu wanaotafuta
kazi, kufundisha utaalamu na pia kuwezesha ushindani katika masuala ya
biashara wataweza kusaidia watanzania kudadavua matatizo yao na kujiweka
mbele katika kufanya mabadiliko ya kiuchumi na kitamaduni ili kusonga
mbele.
Naye Dkt. Reginald Mengi ambaye
ni Mwenyekiti wa makampuni ya IPP na Mwenyekiti wa TPSF alisema kwamba
mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka ambapo serikali imetoa mpango wake
wa maendeleo wa miaka mitano ambao utekelezaji wake unategemea sana
utaalamu na taaluma.
|
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi
ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la
ukaribisho kwa washiriki na wadau wengine katika kongamano hilo.
Alisema kwamba wakati serikali
inajipanga taifa kuwa na uchumi wa kati mwaka 2025 taifa linatakiwa
kujipanga katika kutengeneza rasilimali watu wenye taaluma ambao
wanaweza kulifikisha taifa katika eneo hilo.
Alisema kwamba katika hali hiyo
inafaa kuendelea kuratibu na kutengeneza mitaala inayofaa kwa ajili ya
kuendeleza watu na hivyo kuendeleza taaluma kwa kushirikiana na sekta
binafsi.
Inafaa, alisema Dk Mengi,
utengenezaji wa watu wenye taaluma lazima uende sambamba na haja ya
taifa katika mipango yake ya maendeleo kwa kutoa wataalamu walio bora
ambao watatengeneza bidhaa bora na huduma bora zitakazoinua uchumi wa
mtu mmoja na taifa.
Alisema ipo haja ya kuwapo kwa
ushirikiano wa sekta binafsi na serikali katika kuhakikisha mazingira
yanawezesha uzalishaji zaidi wa wataalamu ambao watakuwa na uhakika na
ubunifu wa kuendeleza teknolojia na kuzitumia kwa ajili ya maendeleo.
Alisema awali uchumi
ulitengenezwa kwa kuzingatia ujamaa ambapo serikali ilikuwa
inafanyabiashara na kuzalisha lakini baada ya mabadiliko inatakiwa vile
vile kubadilika ili kuweza kukidhi mahitaji ya sasa ambayo ni ya soko
huria.
|
Balozi wa Ufaransa nchini, Mh. Malika Berak akizungumza kwenye kongamano hilo.
Aliwataka watanzania kubadilika
katika fikira zao na kuona namna ya kuwezesha maendeleo ya rasilimali
watu kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ambayo yanahitaji utaalamu wa sasa
hasa katika sekta binafsi.
Alisema ni lazima watu pia
katika taaluma lazima kuwepo na uwajibikaji, uadilifu na uwezo katika
kufanikisha maendeleo ya taaluma.
Akitolea mfano wa mtu aliye
mlemavu nchini Japan alitaka watanzania watumie kile kilichopo
tunachoweza ili kutengeneza maisha bora kabisa.
Alisema mlemavu huyo wa Japan
ambaye alikuwa amepooza kuanzia shingoni ambaye kwa sasa ni milionea
alimwambia kwamba alikuwa halilii ambavyo hana bali kile alichonacho
alihakikisha anakitumia vyema.
|
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa
Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald Mengi akifungua kongamano
hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ofisi za ESRF jijini Dar es
Salaam.
Naye Katibu Mkuu Ofisi ya waziri
Mkuu anayeshughulikia Kazi na Ajira, Eric Shitindi katika hotuba yake
iliyosomwa na Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu, Ally Msaki
alisema ipo haja ya wadau wote kuwa pamoja katika kuhakikisha elimu
inaboreshwa na pia wataalamu wanasukwa kwa kuzingatia soko la ajira.
Alisema serikali kwa
kushirikiana na sekta binafsi imechukua hatua kadha kuongeza utaalamu
katika soko la ajira kwa kuanzisha mpango wa miaka mitano ambamo ndani
yake yamezungumzwa masuala ya mafunzo ya ufundi na utaalamu .
Alisema hakuna maendeleo
yanayokusudiwa bila kuwa na wataalamu na hivyo serikali itaendelea
kushirikiana na wadua mbalimbali kuendeleza mafunzo kwa lengo la
kusaidia soko la ajira.
Alisema bila kuwa na ushirikiano
kati ya serikali, sekta binafsi na waajiri hapatakuwapo na wataalamu na
hivyo itakuwa shida katika maendeleo ya taifa.
|
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa pili kushoto) na washiriki wengine wakifuatilia kwa umakini risala ya mgeni rasmi, Dk. Mengi. |
Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu, Ally Msaki akisoma hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi na Ajira, Eric Shitindi katika kongamano hilo. |
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald Mengi (kulia), akibadilishana mawazo na Balozi wa Ufaransa nchini, Mh. Malika Berak (wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kushoto) pamoja na kurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu, Ally Msaki wakati wakielekea kwenye eneo maalum kwa ajili ya zoezi la picha ya pamoja. |
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald Mengi katika picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa kongamano hilo. |
Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Dk. Reginald Mengi (kushoto) akifurahi jambo na Balozi wa Ufaransa nchini, Mh. Malika Berak (wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (katikati) pamoja na Prof. Prosper Ngowi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe kampasi ya Dar es Salaam. |
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kulia) akiagana na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Tonia Kandiero mara baada ya kumalika kwa kongamano hilo. |
No comments:
Post a Comment