Kufuatia kutimiza agizo la uzimaji wa simu bandia, kutokana na agizo elekezi la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA.
Kampuni ya simu za mkononi ya
Airtel inapenda kuwajulisha wateja wake walio nunua simu orijino kutoka
kwa watoa huduma ndani ya maduka yetu ya Airtel, endapo baadhi ya wateja
simu zao zitazima kutokana na agizo hilo. Airtel inawatangazia wateja
wote watakaoathirika na zoezi hili kutembelea maduka yetu nchi nzima
kwaajili ya kuhudumiwa/kurekebishiwa simu zao wakiwa na simu husika
pamoja na risiti za manunuzi ya simu hizo.
Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza kutokana na zoezi hili.
No comments:
Post a Comment