KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 26, 2016

DSE YAKANUSHA MAUZO YA HISA KUATHIRI HALI YA UCHUMI

Kufuatia mijadala iliyotokea katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita iliyolenga kutafsiri kudorola kwa uchumi wa nchi baada ya kupungua kwa idadi ya mauzo katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kwa asilimia 81, soko hilo limefafanua kuwa mauzo yake hayawiani na mwenendo wa uchumi wa nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja Biashara na Mauzo DSE, Patrick Mususa amefafanua kuwa kiashiria hicho hakikuwa sahihi katika kutafsiri hali ya uchumi wa nchi.
Mususa amesema sababu iliyopeleka idadi ya mauzo kushuka ni kutokana na kupungua kwa uhitaji pamoja na kushuka kwa bei za hisa kwa wiki husika.
“Hakuna uhusiano na uwiano baina ya idadi ya mauzo ya soko la hisa na uchumi wa nchi, na mauzo ya soko hilo si kiashiria sahihi kutumiwa katika kutafsiri mwenendo wa uchumi wa nchi,” amesema na kuongeza.
“Wiki iliyopita punguzo la idadi ya mauzo ya hisa ilikuwa asilimia 81 ambapo ilikuwa bilioni 1.7 idadi ilipungua kwa sababu wiki iliyopita ilikuwa fupi yaani ilikuwa na siku nne za kazi, pia soko huwa linaendeshwa na wanahisa wenyewe ambao huangalia mahitaji yao husika hivyo kushuka kwa idadi ya mauzo kuna tegemea na bei husika ya hisa na mahitaji yake kwa wiki hiyo,”
Aidha Mususa amesema kuwa DSE haina kampuni za kutosha zinazowakilisha sekta nyeti zinazoshikilia uchumi kutokana kwamba takribani kampuni 17 za ndani ndizo zilizoorodheshwa.
“Hakuna kampuni za kutosha ili kutafsiri uwiano wa uchumi wa nchi, mfano DSE haina kampuni za simu ina maana sekta ya mawasiliano haijaorodheshwa, kwa upande wa sekta ya viwanda kampuni za simenti, bia na sigara ndizo zilizoorodheshwa pekee,”
Hata hivyo, Mususa amesema kuna ongezeko la mauzo ya idadi ya hisa kwa wiki iliyopita zaidi ya mara tisa na kufikia bilioni 16.4 kutoka bilioni 1.7.
“Ukubwa wa mtaji wa soko uneongezeka kwa asilimia 3.9 kutoka trilioni 20.8 hadi 21.6 trilioni.” amesema.
Mususa amewataka wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa kuorodhesha kampuni zao katika soko hilo ili kuongeza mitaji ya kampuni zao.
“Wafanyabiashara na jamii kwa ujumla tunawashauri kushirikiana na DSE ili kupata fursa ya kujitangaza, na kupata mitaji,” amesema

No comments:

Post a Comment