KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

December 7, 2016

VIKUNDI 26 VYA UJASIRIAMALI VYAWEZESHWA CHALINZE


pioo
Diwani wa kata ya Kibindu Ramadhani Mkufya ,akizungumza kabla ya vikundi vya ujasiriamali vilivyopo kwenye kata yake kupatiwa hundi ya mkopo kutoka halmashauri ya Chalinze.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
ret
Afisa vijana na maendeleo ya jamii katika halmashauri ya Chalinze,Felister Kizito,akizungumza baada ya kukabidhi hundi za mkopo kwa makundi mbalimbali ya ujasiriamali jimbo hapo(Picha na Mwamvua Mwinyi)
ret-1
Mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze ,Saidi Zikatimu akizungumza na wananchi na watu waliojiunga katika vikundi vya ujasiriamali katika kata ya kibindu.(Picha na Mwamvua Mwinyi) 
………………
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
HALMASHAURI ya Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani imetumia kiasi cha sh.mil 79.5 ,kuwezesha  vikundi 26,vya wajasiriamali wanawake na vijana katika kata mbalimbali.
Aidha halmashauri hiyo imepanga kuviwezesha vikundi vya ujasiriamali 200  kwa kipindi cha mwaka mmoja ujao ili kuwaongezea mitaji na kuwainua  kiuchumi . Akikabidhi fedha hizo katika vikundi hivyo,mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze,Saidi Zikatimu alisema ,fedha hizo zimetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya robo mwaka  kiasi cha sh.mil 809 ambayo yalikusanywa.
Alieleza kwamba upande wa kundi la wanawake wamepatiwa asilimia tano na vijana asilimia tano kati ya asilimia 10 iliyotengwa.
Zikatimu alisema lengo la kutolewa fedha hizo ni kuwawezesha wanawake na vijana kiuchumi ili kujiendeleza kimaisha .
“Lengo jingine ni kufuata sheria ambayo inataka asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri yakopeshwe makundi hayo ya vya uzalishaji mali”alisema Zikatimu.
Hata hivyo mwenyekiti huyo alifafanua kuwa kwa kipindi hiki cha robo ya mwaka wamekusanya mil.809 katika mapato ya ndani ambapo mil.258 wametenga kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Zikatimu aliwaomba wajasiliamali hao kurejeshe fedha kwa wakati ili ziweze kuzungushwa katika makundi mengine ambayo bado hayajapatiwa mikopo kwa kipindi hiki.
‘Mrejeshe kwa wakati fedha hizi na mhakikishe mnazitumia kwa malengo lengwa sio tena mchezee ngoma,wanaume muolee wake wenza ama kulewea pombe la hasha ” alisema Zikatimu.

No comments:

Post a Comment