KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

December 7, 2016

YANGA YATANGAZA KUACHA NA MBUYU TWITE RASMI

 

acha

Na.Alex Mathias

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara klabu ya Yanga imethibitisha rasmi kuachana na kiungo mkabaji mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi uwanjani,Mbuyu Twite na nafasi yake kuchukuliwa na kiungo mkabaji Justine Zullu toka timu ya Zesco United ya nchini Zambia.

Licha ya kuachana na klabu hiyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi uwanjani anaondoka kwa amani na akiacha maneno mazito nyuma yake.

“Yanga ni kama familia kwangu daima itabaki moyoni mwangu na kumbuka mashabiki walivyofurika kuja kunipokea siku ambayo niliwasili kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo na ni wakati sasa wa kuwapisha vijana ili kuleta changamoto mpya ili kuipeleka mbele zaidi klabu hii pale tulipoishia sisi”alisema Twite

Mbuyu Twite alijiunga na Yanga msimu wa 2013-14 akicheza vyema nafasi zote za ulinzi na kusimama kama kiungo mkabaji kwa muda mrefu na ikumbukwe usajili wake ulileta kelele nyingi kutokana na kuwa Simba nao walitoa pesa za usajili wa mchezaji huyu ila Yanga waliwazunguka watani zao na kumpandia dau na kuwazidi kete.

Kiraka huyu anaondoka Yanga akiwa na medali za ubingwa wa ligi kuu mwaka 2014-15 na 2015-16,Ngao ya Jamii 2014 na 2015 na pia atakumbukwa kwa kuweka rekodi ya kuipeleka timu hiyo katika hatua ya makundi ya Michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Kumekuwa na taarifa kuwa kiungo huyu atajiunga na mahasimu wao wakubwa nchini Tanzania timu ya Simba kwa sasa Yanga ipo chini ya kocha mpya George Lwandamina raia wa Zambia ambaye amechukua mikoba ya Kocha Hans Van Der Pluijm ambaye amepandishwa cheo na kuwa Mkurugenzi Mkuu wa klabu hiyo na kuna taarifa za chini kuwa mshambuliaji Obrey Chirwa huenda akatolewa kwa mkopo kwenda klabu yake ya Zamani FC Platinum na kupisha usajili wa mshambuliaji ambaye anatajwa kuja Yanga kwa ajili ya kuimarisha kikosi katika michuano ya klabu bingwa Afrika inayotarajiwa kuanza Februari Mwakani.

No comments:

Post a Comment