Mkuu wa Chuo cha Taifa cha
Usafirishaji (NIT)Prof.Zacharia Mganilwa akimuonesha Naibu Mkurugenzi
Mtendaji wa TAZARA Bw. Betram Kiswaga maeneo mbalimbali ya chuo hicho
wakati wa kongamano lililowakutanisha wanafunzi waliowahi kusoma katika
chuo hicho katika miaka ya nyuma na waliomaliza mwaka ulioisha wa
masomo.
Baadhi wa wahitimu na wanafunzi
waliowahi kusoma katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wakiwa
katika kongamano lililowakutanisha na viongozi wa chuo hicho.
Mkuu wa Chuo cha Taifa cha
Usafirishaji (NIT) Prof.Zacharia Mganilwa akiongea na wahitimu na
wanafunzi waliowahi kusoma katika Chuo hicho ambapo alisema dhumuni la
kuwakutanisha ni kutoa zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika
masomo yao ikiwa ni lengo la kuongeza ufaulu na kuwa na wanafunzi bora
ambao wanaweza kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa nchi kwa kutumia
elimu waliyoipata kutoka chuoni hapo.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa
TAZARA Bw. Betram Kiswaga akiongea na na wahitimu na wanafunzi waliowahi
kusoma katika Chuo hicho ambapo alisema taasisi yake itaendelea
kuonesha nia ya kukisaidia chuo hicho ili kiendelee kukua zaidi na kutoa
wahitimu bora katika soko la ajira nchini na afrika kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment