Mwenyekiti
wa Good News For All Ministry , Askofu Dkt. Charles Gadi (kulia)
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu utendaji
wa kazi wa Rais John Pombe Magufuli na kumshukuru kwakupiga vita
uingizwaji, uuzwaji na matumizi ya dawa za kulevya hapa nchini
(katikati), Askofu Ernest Sumisumi wa Kanisa la Baptist, na kushoto
Askofu Hezron Mwasemba wa Kanisa la Mafuta.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWEBLOG
|
Maaskofu wakiwa wameshika picha ya rais John Pombe Magufuli kwa ajili ya maombezi maalumu. |
Maaskofu wakiwa wamenyanyua picha ya rais John Pombe Magufuli kwa ajili ya maombezi. |
Baadhi
ya waandishi wa habari wakimsikiliza askofu Dkt. Charles Gadi (hayupo
pichani) wakati alipokuwa akizungumza kuhusu jukumu la Rais John Pombe
Magufuli kupiga vita matumizi na uuzwaji wa Madawa ya kulevya jijini Dar
es Salaam.
Watanzania
wametakiwa kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na utendaji wake wa kazi hasa
katika zoezi gumu la kupiga vita madawa ya kulevya.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwenyekiti wa Good News For
All Ministry , askofu Dkt. Charles Gadi kwa niaba ya madhehebu
mbalimbali, amesema utendaji wa rais John Pombe Magufuli unapaswa
kuungwa mkono na kila mtanzania kwani vita ya dawa za kulevya ni kubwa
na ngumu kuzizibiti lakini kwa mwenendo alioanzia mhe rais ni mzuri na
atashinda vita hivyo.
Aidha askofu Dkt. Charles Gadi aliongoza jopo la maaskofu wenzake kumuombea rais Magufuli, taifa pamoja na viongozi wengine.
|
No comments:
Post a Comment