Beki kisiki wa kati
wa Azam FC, Aggrey Morris jana jioni alianza rasmi mazoezi mepesi ya
kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya mabingwa watetezi, Yanga.
Hiyo, ikiwa ni siku
moja tangu washambuliaji wa Yanga Mzimbabwe, Donald Ngoma na Mrundi,
Amissi Tambwe wapone majeraha ya goti na kuanza mazoezi ya kujiandaa na
mchezo huo.
Timu hizo,
zinatarajiwa kuvaana Aprili Mosi, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam katika mchezo unaotarajiwa kujaa upinzani mkubwa.
Morris alisema
anarejea uwanjani baada ya kupata nafuu ya majeraha yake ya mfupa wa
paja la kulia wakati timu hiyo ilipocheza mchezo wake wa Kombe la
Shirikisho Afrika dhidi ya Mbabane Swallows ya Swaziland.
“Namshukuru Mungu
kwa kuweza kurejea uwanjani kwa sababu mchezaji lengo lake ni kucheza na
siyo kukaa tu, hamna kitu kibaya kwa mchezaji kama kupata majeraha
yatakayosababisha kumuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu.
“Hivyo, hivi sasa
nimepata nafuu ya majeraha yangu na kuanza mazoezi mepesi ya binafsi
kabla ya kuanza programu ya mazoezi magumu na wenzangu katika kujiandaa
na mechi dhidi ya Yanga,” alisema Morris.
|
March 29, 2017
AGGREY MORRIS FITI KUWAVAA YANGA JUMAMOSI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment