Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe leo
amezungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma mara baada ya
kukaribishwa rasmi Wizarani hapo..
Baada
ya maongezi aliruhusu mwaswali ambapo moja ya swali aliloulizwa na
wanahabari ni kuhusu ripoti iliyoachwa na Waziri wa zamani Nape Nnauye
kuhusu uchunguzi wa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kudaiwa
kuvamia ofisi za Clouds Media huku akiwa na Askari wenye silaha.
==>Haya ni majibu aliyoyatoa
"Wengi
mnauliza nimeifanyia kazi gani ripoti ya Nape, mimi hiyo ripoti
sijaiona na kama mwanasheria kwangu ni mwiko na sitapeleka taarifa
ambayo haijakamilika.
"Kupitia
vyombo vya habari taarifa imeeleza kuwa ushahidi ulitolewa na upande wa
Clouds Media na mkakiri kuwa upande wa pili haukupatikana.
"Huwezi
kuwa Hakimu kwenye suala lako wewe mwenyewe, kufanya hivyo ni ubatili
kwahiyo hata mimi ningekuwa ni mwandishi wa habari ningesema hili jambo
siliwezi kwakuwa linanihusu na mimi.
"Kanuni
zinataka kusikiliza upande wa pili, sasa mmeshasema kitu kina upande
mmoja alafu nimpelekee kiongozi wangu..NO, mimi kazi yangu ni kupata
maelezo ya upande wa pili na nitapata.
"Hili
jambo ni lakufa na kupona, yani niache kukutana na wakuu wa idara
mbalimbali hapa kuhakikisha nakuza suala la sanaa na kuhakikisha vijana
wetu hawaendelei kuibiwa nibaki kuhangaikia suala la ripoti.
"Mimi
sikuapa kwa jambo hilo moja pekee lakini mimi ni mwanasheria mkongwe na
nitahakikisha nalifuatilia lakini mimi sitaunda kamati katika jambo
hilo.
"Lengo
letu ni kuhakikisha hatutakuwa na matukio ya namna hiyo katika safari
lakini tukitoka na kauli za papara tutakuwa tunajitafutia matatizo hapo
mbeleni "
|
March 29, 2017
MWAKYEMBE:HUWEZI KUWA HAKIMU WA KESI YAKO MWENYEWE....RIPOTI YA UVAMIZI WA CLOUDS MEDIA INA MAPUNGUFU,SITAIPELEKA NGAZI ZA JUU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment