Kocha wa Timu ya Kagera Sugar Meck Mexime ambaye amewahi pia kuwa kocha wa Mtibwa Sugar amesema Mchezaji Mohamed Fakhi hakuwa na KADI tatu za Njano kama Simba wanavyodai na kukata Rufaa ili kupata points tatu za Mezani.
Mexime amesema " Nadhani kila mtu aliona tuliwafunga Simba, Na mchezo wa mpira huwa unachezwa hadharani na Kulingana na rekodi zetu Mchezaji Mohamed Fakhi alikuwa na kadi mbili za Njano Pekee "
Inadaiwa Simba wamekata Rufaa wamekata Rufaa ili kupata Points Tatu za mchezo huo ambao ulimalizika kwa Simba kufungwa bao 2 kwa 1.
Hata Hivyo kamati ya masaa 72 imesema itatoa majibu ya Rufaa hiyo Alhamisi Ijayo.
No comments:
Post a Comment