KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 19, 2017

RONALDO AIPELEKA REAL MADRID NUSU FAINALI NA LEICESTER CITY YATUPWA NJE LIGI YA MABINGWA

1492547381474_lc_galleryImage_Real_Madrid_s_Portuguese_
Mshambuliaji wa Real Madrid na Nahodha wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amefikisha mabao 103 aliyofunga katika michuano ya Ulaya ngazi ya klabu huku  akiingia uwanjani akiwa na mabao 100 baada ya kufunga mawili mjini Munich.

Bayern walianza kufunga bao la kwanza dakika ya 53 kwa mkwaju wa penalti kupitia Robetro Lewandowski, Madrid wakasawazisha dakika ya 76 akifunga Ronaldo kabla ya beki Sergio Ramos kujifunga dakika mbili baadaye.


Kipigo cha 2-1 kwa Madrid kilisababisha kuongezwa kwa dakika 30 na ndipo Madrid ilipoanza kuporomosha mvua ya mabao, Ronaldo akifunga dakika ya 106 kwa pasi ya Ramos na Marcelo akawachambua mabeki wanne kabla ya kumpa pasi safi Ronaldo aliyefunga bao la nne dakika ya 110.

Marco Asensio ndiye aliyefunga bao la nne katika dakika ya 112 na kumaliza kazi dhidi ya Bayern ambao walicheza pungufu kuanzia dakika ya 84 baada ya Arturo Vidal kupigwa “umeme”.


Real Madrid starting XI: Navas; Carvajal, Ramos, Nacho, Marcelo; Casemiro, Kroos, Modric; Isco, Benzema, Ronaldo
Substitutes: Kiko Casilla, James, Kovacic, Lucas Vazquez, Asensio, Morata, Danilo

Bayern Munich starting XI: Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Alaba, Robben, Alonso, Vidal, Thiago, Ribery, Lewandowski 
Substitutes: Ulreich, Bernat, Kimmich, Costa, Rafinha, Coman, Muller.

MATOKEO MENGINE

Leicester City imeaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Atletico Madrid.

Leicester ndiyo waliokuwa nyumbani na walilazimika kusawazisha kwa bao la Jammy Vardy ili kupata sare hiyo.


Kwa sare hiyo, maana yake Atletico Madrid imesonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya ushindi wa 1-0 ikiwa nyumbani Vicente Cardelon jijini Madrid.

KIKOSI CHA Leicester City:
Schmeichel, Simpson, Morgan (Amartey), Benalouane (Chilwell), Fuchs, Mahrez, Ndidi, Drinkwater, Albrighton, Okazaki (Ulloa), Vardy

KIKOSI CHA Atletico Madrid:
 Oblak, Juanfran (Hernandez), Savic, Godin, Filipe Luis (Correa), Saul, Gabi, Gimenez, Koke, Carrasco (Torres), Griezmann

No comments:

Post a Comment