Mshambuliaji wa Real
Madrid na Nahodha wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amefikisha
mabao 103 aliyofunga katika michuano ya Ulaya ngazi ya klabu huku
akiingia uwanjani akiwa na mabao 100 baada ya kufunga mawili mjini
Munich.
Bayern walianza
kufunga bao la kwanza dakika ya 53 kwa mkwaju wa penalti kupitia Robetro
Lewandowski, Madrid wakasawazisha dakika ya 76 akifunga Ronaldo kabla
ya beki Sergio Ramos kujifunga dakika mbili baadaye.
Kipigo cha 2-1 kwa
Madrid kilisababisha kuongezwa kwa dakika 30 na ndipo Madrid ilipoanza
kuporomosha mvua ya mabao, Ronaldo akifunga dakika ya 106 kwa pasi ya
Ramos na Marcelo akawachambua mabeki wanne kabla ya kumpa pasi safi
Ronaldo aliyefunga bao la nne dakika ya 110.
Marco Asensio ndiye
aliyefunga bao la nne katika dakika ya 112 na kumaliza kazi dhidi ya
Bayern ambao walicheza pungufu kuanzia dakika ya 84 baada ya Arturo
Vidal kupigwa “umeme”.
Real Madrid starting XI: Navas; Carvajal, Ramos, Nacho, Marcelo; Casemiro, Kroos, Modric; Isco, Benzema, Ronaldo
Substitutes: Kiko Casilla, James, Kovacic, Lucas Vazquez, Asensio, Morata, Danilo
Bayern Munich starting XI: Neuer, Lahm, Boateng, Hummels, Alaba, Robben, Alonso, Vidal, Thiago, Ribery, Lewandowski
Substitutes: Ulreich, Bernat, Kimmich, Costa, Rafinha, Coman, Muller.
MATOKEO MENGINE
Leicester City imeaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Atletico Madrid.
Leicester ndiyo waliokuwa nyumbani na walilazimika kusawazisha kwa bao la Jammy Vardy ili kupata sare hiyo.
Kwa sare hiyo, maana yake Atletico Madrid
imesonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya ushindi wa 1-0 ikiwa
nyumbani Vicente Cardelon jijini Madrid.
KIKOSI CHA Leicester City:
Schmeichel, Simpson, Morgan (Amartey),
Benalouane (Chilwell), Fuchs, Mahrez, Ndidi, Drinkwater, Albrighton,
Okazaki (Ulloa), Vardy
KIKOSI CHA Atletico Madrid:
Oblak, Juanfran (Hernandez), Savic, Godin, Filipe Luis (Correa), Saul, Gabi, Gimenez, Koke, Carrasco (Torres), Griezmann
No comments:
Post a Comment