Mahakama ya Rufaa nchini Kenya
imebatilisha uamuzi wa Mahakama Kuu uliokuwa umefuta kandarasi ya kupiga
chapa karatasi za kura za urais kufuatia kesi iliyokuwa imewasilishwa
na muungano wa upinzani.
Majaji wa mahakama ya rufaa wamesema
mahakama hiyo ya chini ilikosea ilipoamua kwamba wananchi walifaa
kushirikishwa katika uamuzi wa kutoa kandarasi hiyo ya thamani ya $24m
(£18m) kwa kampuni ya Al Ghurair kutoka Dubai.Mahakama hiyo imesema si lazima kwa taasisi ya serikali inapoamua kutoa zabuni moja kwa moja kushirikisha wananchi katika kufanya uamuzi au hata kufikia uamuzi wenyewe wa kutumia njia hiyo kutoa kandarasi hiyo. Aidha, majaji hao wamesema mahakama ilifaa kuzingatia maslahi ya wananchi na haki yao ya kushiriki katika uchaguzi huru na wa haki. Wamesema ni lazima uchaguzi mkuu ufanyike tarehe 8 Agosti na majaji wa Mahakama Kuu walifaa kuzingatia muda uliopo kwa Tume ya Uchaguzi (IEBC) kujiandaa ili kufanikisha uchaguzi huo. |
July 20, 2017
TUME YA UCHAGUZI YA KENYA YASHINDA RUFAA KUHUSU KARATASI ZA KURA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment