KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 21, 2017

WATAALAM WAONMYA KUHUSU ROBOTO ZINAZOUA

A robot distributes promotional literature calling for a ban on fully autonomous weapons in Parliament Square, London, 23 April 2013
Wataalamu hao 116 wametaka kuwekwa marufuku ya kutumia teknolojia hiyo kuunda roboti inayoweza kutumiwa kama silaha.
Zaidi ya wataalamu 100 wa teknolojia ya roboti wameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua ili kuzuia kundwa wa roboti zinazoweza kuua.
Kwenye barua kwa Umoaj wa Mataifa, wataalamu wa masuala ya teknolojia akiwemo tajiri Elon Musk, wameonya kuwa hatua hiyo itasababisha kuwepo kwa vita vitakavyohusisha roboti.
Wataalamu hao 116 wametaka kuwekwa marufuku ya kutumia teknolojia hiyo kuunda roboti inayoweza kutumiwa kama silaha.
"Wakati zitaundwa, zitawezesha vita kupiganwa kwa kiwango kingine cha juu na kwa haraka zaidi kuliko vile binadamu hufanya." barua hiyo ilisema.
"Hizi zitakuwa silaha za ugaidi, silaha ambazo magaidi watatumia dhidi wa watu wasio na hatia, na silaha ambazo zitadukuliwa kuhudumu kwa njia ambayo sio nzuri." iliongeza.
Mwaka 2015 zaidi ya wataalamu 1,000 na watafiti waliandika barua wakionya kuhusua kuundwa kwa silaha kama hizo.
Kati ya wale walioweka sahihi barua ya mwaka 2015 ni mwanasayansi Stephen Hawking, na mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Apple Steve Wozniak na bwana Musk.

Roboti za kuua ni zipi?

Roboti za kuua ni silaha ambazo zinaweza kuchagua na kuvamia kitu ambacho zinakilenga bila ya kuelekezwa na binadamu. Tayari kwa sasa zipo lakini kuboreshwa zaidi kwa teknolojia itachangia kuziwezesha kufanya hivyo.
Wale wanaopendelea roboti hizo wanaamini kuwa sheria za sasa za vita zinatosha kutatua shida yoyote ambayo itaibuka ikiwa zitatumiwa.
Lakini wale wanaozipinga wanasema kwa roboti hizo ni tisho kwa binadamu na teknolojia yoyote ya kuziwezesha kuuwa inastahili kupigwa marufuku. CHANZO BBC
  

No comments:

Post a Comment