Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt.
Augustine Mahiga akizungumza na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala
ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory
alipofika Wizarani tarehe 22 Agosti, 2017 kwa ajili ya mazungumzo rasmi
na Waziri Mahiga. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa
kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Uingereza.
Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lale la Kimataifa la Maendeleo
(DFID) inaisadia Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo
Maji, Elimu, Nishati Mbadala na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.
Mhe. Stewart yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 22 na
23 Agosti, 2017. |
No comments:
Post a Comment