Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi Dkt.
John Pombe Magufuli, ametangaza kutoa ajira kwa wanajeshi 3000 wapya
mwaka huu, ili jeshi la Tanzania liweze kuwa na askari wa kutosha.
Rais
Magufuli ametoa taarifa hiyo leo alipokuwa akihutubia umma mara baada
ya kuwapa kamisheni maafisa wa Jeshi, katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid
mkoani Arusha, huku akitaka wahusika kutowasahau vijana waliohitimu
mafunzo ya JKT.
"Lakini
pia leo tumepata maofisa 422, unapokuwa na jeshi la maofisa lazima
kuwepo na 'junior officers', huwezi ukawa na jeshi lote lina maofisa,
kwa kutambua hili natangaza rasmi kwamba nitatoa nafasi 3,000 za kuajiri
wanajeshi wapya, na hawa wataoajiriwa muzingatie na wale ambao
wamemaliza JKT, lengo ni kuhakikisha jeshi letu linakuwa na maaskari wa
kutosha na la kisasa zaidi", amesema Rais Magufuli.
Leo
Rais Magufuli ametoa kamisheni kwa Maafisa wa Jeshi 422 waliohitimu
mafunzo katika chuo cha Monduli, hafla ambayo imekuwa ya kwanza
kufanyika katika uwanja wa umma,
No comments:
Post a Comment