KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 22, 2017

MBAO FC YAIVURUGA SIMBA UWANJA WA CCM KIRUMBA

DSC_9754-640x426
Timu ya Mbao FC imekuwa ya kwanza kuifunga Simba magoli mawili tangu msimu uanze kwani imeweza kucheza mechi tatu bila kuruhusu nyavu kutikiswa Mchezo uliomalizika kwenye uwanja wa CCM Kirumba kwa kutoka sare ya 2-2 Mzunguko wa nne wa  Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara .
Simba walimudu kucheza mechi tatu bila kuruhusu bao katika nyavu zao huku Aishi Manula akiwa amecheza kwa zaidi ya dakika 325 bila kufungwa.
Hii imekuwa ya pili kwa Simba huku ikiwa ya kwanza kwa Mbao FC baada ya kucheza mechi nne ,ikishinda moja,sare moja na kufungwa Miwili huku Vijana wa Omog wakishinda mechi mbili na kutoka sare mbili.
Mchezo uliochezeshwa na refa Athumani Lazi wa Morogoro, hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililofungwa na winga machachari, Shiza Ramadhani Kichuya dakika ya 16 akimalizia krosi nzuri ya beki Erasto Edward Nyoni. Kichuya alishindwa kuendelea na mchezo dakika ya 44 baada ya kuumia na kumpisha Haruna Niyozima, wakati Mbao nalo walimtoa Said Said dakika ya 37 na kumuingza Herbet Lukindo. Kipindi cha pili Mbao walirudi kwa kasi nzuri na kufanikiwa kusawazisha bao dakika ya 46 tu, kupitia kw3a Habib Kiyombo ambaye hilo linakuwa bao lake la tatu msimu huu. Hata hivyo, Simba walijibu kwa mashambulizi mfululizo na kufanikiwa kupata bao la pili dakika tatu baadaye, mfungaji kiungo Mghana, James Kotei.    Mbao hawakukata tamaa, waliendelea kushambulia na kufanikiwa kusawazisha tena dakika ya 81 kupitia Emmanuel Mvuyekire aliyefunga kwa shuti la mbali pia. Hadi mwamuzi anamaliza Mpira timu hizo zimeweza kugawana alama huku Simba wakibaki kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi 8 na Mbao Fc wamefikisha jumla ya Pointi 4,Ligi Kuu ya Vodacom itaendelea wikendi hii na kinara bado anaongoza Mtibwa Sugar wenye pointi 9 ambao hawajapoteza hata mechi moja .

No comments:

Post a Comment