Kikundi cha
ngoma yaasiliya Sindimba toka mkoa wa Mtwara,Wakicheza ngoma hiyo jana wakati wamashindano ya ngoma za asili yaliyodhaminiwana
Vodacom Tanzania PLC ya”Tulia Traditional dances festival 2017”yanayofanyika
kwa siku tatu katika viwanja vya tandale mjini tukuyu wilayaya Rungwe mkoa wa Mbeya.
TAMASHA la ngoma
za kitamaduni lililopewa jina la Tulia Traditional Dance Festival, limeanza kwa
mbwembwe mjini Tukuyu, mkoani Mbeya jana, likishirikisha vikundi zaidi ya 100
kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini ambapo litafikia tamati kesho.
Akizungumza tamasha
hilo akiwa Tukuyu jana, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Tulia Ackson ambaye ndiye mwasisi wake, alisema kuwa
anajisikia furaha kuona tukio hilo limepokewa vizuri mno na wakazi wa Tukuyu na
mkoani Mbeya, lakini pia na Tanzania kwa ujumla.
“Maandalizi yanaendelea
vizuri na mwitikio umekuwa mkubwa mno kuonyesha jinsi Watanzania wanavyothamini
tamaduni zao. Matamasha kama haya ni muhimu mno kwani hutoa fursa ya kutangaza
utamaduni wetu wa kitanzania na kuwa moja ya kivutio badala ya kutegemea
vivutio vya kiutalii vilivyozoeleka kama Mlima Kilimanjaro, mbuga na hifadhi za
wanyama na vinginevyo.
“Nawaomba
wabunge waandae matamasha kama haya katika maeneo yao ili baadaye washindi
watakaopatikana, waweze kushiriki katika tamasha letu hili ili kulifanya kuwa
la kitaifa zaidi, hii itasaidia kuwaonyesha vijana wetu wa kizazi cha sasa kufahamu
tamaduni zao, kuona mababu zao walikuwa wakifanya nini.
“Kwa serikali,
iandae na kuunga mkono matamasha ya utamaduni kama sehemu ya kuenzi utamaduni
wetu kwani vijana wengi wamekuwa wakibobea katika tamaduni za kigeni kutokana
na kutofahamu tamaduni zao,” alisema.
Aliipongeza
kampuni ya Vodacom kwa kujitosa kudhamini tamasha hilo la aina yake ambalo anaamini
litafana vilivyo mwaka huu.
Alisema tamasha
hilo limeshirikisha vikundi zaidi ya 100 kutoka mikoa mbalimbali, hali inayotoa
picha kuwa kwa sasa ni tukio la kitaifa, akiwataka wanasiasa, hasa wabunge,
mashirika, taasisi na kampuni mbalimbali kujitokeza kulidhamini.
Kwa upande wake,
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mwori,
alisema kuwa huu ukiwa ni mwaka wao wa kwanza kudhamini tamasha hilo,
wanajisikia fahari kubwa kuungana na Muheshimiwa Dk Tulia kusapoti tukio hilo,
wakiwa kama miongoni mwa wadau wa masuala ya burudani, michezo na mambo ya
kijamii.
“Vodacom
Tanzania tunajisikia fahamu kuwa sehemu ya tamasha hili kupitia udhamini wetu,
tumeona ni vema kudhamini tamasha hili kwani lina manufaa makubwa kwa jamii ya
kitanzania, hasa katika suala zima la kuuenzi utamaduni wa Mtanzania,” alisema.
Aliongeza: “Kama
kila mmoja wetu anavyofahamu, Vodacom Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika
kusapoti matukio mbalimbali ya kijamii kama sehemu ya kuionyesha jamii jinsi
tunavyoijali kwani ndio wadau wetu wakubwa waliotuwezeshja leo hii kuwa mtandao
bora kabisa wa mawasiliano hapa nchini.”
Alisema kama
ambavyo wamekuwa wakisapoti matukio mbalimbali ya kimichezo na utamaduni kama
vile udhamini wao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, mashindano ya Dance 100% na mengineyo, wataendelea kudhamini tamasha
hilo miaka ijayo kadri itakavyowezekana.
Aliwataka wadau
wengineo wa sanaa na burudani kwa ujumla hapa nchini kujiotokeza kudhamini
tamasha hilo ambalo anaamini linaweza kuwa dira ya utamaduni wa Mtanzania iwapo
litapewa sapoti inayostahili.
Naye mkazi wa
Iromba, Mbaye ambaye amehudhuria tamasha hilo, Kenneth Sanga, alilimwagia sifa
tamasha hilo akisema kuwa linakumbusha tulikotoka likitoa fursa kwa vijana wa
sasa kufahamu watu wa zamani walikuwa wakifanya nini.
“Kuna watu wa
kutoka maeneo mbalimbali wamehudhuria tamasha hili, hili ni jambo kubwa sana
hivyo ni vema serikali ikaunga mkono jitihada hizi zilizoonyeshwa na
muheshimiwa Dk Tulia kwa kuendesha matamasha kama haya katika maeneo mbalimbali
nchini,” alisema Sanga.
|
No comments:
Post a Comment