Jeshi
la Polisi kanda Maalumya Dar es Salaam limekamata silaha mbalimbali
zikiwemo bunduki, bastola na vifaa vingine vya kufanyia matukio ya
uhalifu pamoja na watuhumiwa mbalimbali wa makosa ya uhalifu ambao
walikuwa wakijiandaa kutekeleleza matukio hayo.
Akizungumza
na wanahabari ofisini kwake leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar,
Lazaro Mambosasaamesema jeshi hilo limekamata silaha aina ya AK 47 na
watuhumiwa wawili nyumbani kwa mzee Said Omary (62) baada ya kupata
taarifa kuwa kuna wahalifu wanataka kufanya tukio la wizi wa kutumia
silaha.
Aidha
Polisi imewakamata watuhumiwa 2 wa wizi wa magari ambao baada ya
kufanyiwa upekuzi walikutwa na radio call, kadi 10 za benki mbalimbali,
leseni za udereva, master keys 15 ambapo baada ya kuhojiwa walikiri
kutekeleza matukio mbalimbali ua uhalifu huku wakionesha magari mawili
na pikipiki moja vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi.
No comments:
Post a Comment