Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH) jana imewaruhusu Maria na Consolata waliokuwa
wamelezwa katika hispotali hiyo kwa zaidi ya miezi miwili kutokana na
afya zao kuimarika.
Pacha
hao walikuwa wakipatiwa matibabu na madaktari bingwa wa Muhimbili na
jana wamepelekwa Iringa ambako watapokelewa na Mganga Mkuu wa Hospitali
ya Mkoa wa Iringa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru amesema pacha hao
wamesindikizwa na madaktari wa Muhimbili had Iringa na kwamba wakiwa huo
wataendelea kupatiwa matibabu.
“Consolata
na Maria tumewaruhusu . Hii ni baada ya madaktari kujiridhisha kwamba
afya zao zimeimarika. Wataalamu wetu wamewafanyia vipimo mbalimbali na
pia tumewasiliana na wenzetu wa nje na tukakubaliana tuwaruhusu sasa,”
alisema Prof. Museru.
Prof.
Museru alisema kwamba pacha hao wamepatiwa machine ya CPAP & Oxygen
ambayo itawasaidia kuwapatia tiba endapo watahitaji wakati wakiwa
Iringa.
Wakizungungumza
kwa nyakati tofauti, Consolata amesema kwamba Muhimbili imewapatia
huduma nzuri na wanawashukuru wataalamu mbalimbali waliokuwa wakiwapatia
matibabu tangu walipolazwa.
Naye
Maria akizungumza kwa furaha amesema hivi sasa anajisikia vizuri
tofauli na awali-kabla ya kupelekwa katika hispotali hiyo kwa ajili ya
matibabu. Pia, amemshukuru mkurugenzi mtendaji wa Muhimbili kwa
kuwapatia huduma bora za matibabu.
No comments:
Post a Comment