KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 28, 2018

WAAJIRI LETENI WATUMISHI WANOLEWE TPSC- MKUCHIKA



Na Mwandishi Wetu,Mbeya

Serikali imeendelea kuwasisitiza waajiri wote nchini kuwapeleka watumishi 
wao Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kupigwa ‘msasa’ namna ya kufanya kazi za utumishi wa umma.

Akizungumza jijini hapa mwishoni wa wiki wakati wa Mahafali ya 28 ya TPSC Waziri wa nchi- Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt (Msaafu) George Mkuchika alisema kuwa ni muhimu waajiri hao wakawapeleka watumishi chuoni hapa hasa ikitiliwa maanani kwamba TPSC ndiyo chuo kilichopewa dhamana ya kuendesha mafunzo ya awali na elekezi kwa waajiri wapya wa serikali.

Alisema pamoja na makujuku hayo pia Chuo hicho kina wajibu wa kusimamia mitihani ya utumishi wa umma katika program ya kuendeleza watumishi.

Pia TPSC inatoa mafunzo ya kozi nyingine za muda mrefu na mfupi katika maeneo ya uongozi, Utawala na ya matumizi ya mifumo ya kisasa ya TEHAMA.

Waziri Mkuchika aliwaasa wahitimu kwamba mafunzo waliyoyapata chuoni hapo yasiishie kwenye vyeti bali yawe ni mafunzo ya kufanya kazi kwa weledi na kasi mpya yenye ufanisi wa ili kuleta tija kwa lengo kukuza uchumi wa taifa hili.

“Ninawasihi huu usiwe mwisho wa kujiendeleza kwani mafunzo huongeza ujuzi , weledi na mbinu maridhawa za ufanisi wa kazi hususan katika kujifunza teknolojia mpya,” alisema.

Waziri wa nchi- Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt (Msaafu) George Mkuchika akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa Mahafali ya 28 ya TPSC chuoni hapo Jijini Mbeya.
Mtendaji Mkuu wa TPSC Dkt Henry Mambo akizungumza wakati wa Mahafali hayo ya 28 ya TPSC Jijini Mbeya
Baadhi ya wahitimu wa Mahafali ya 28 ya TPSC wakiwa kwenye mahafali hayo chuoni hapo Jijini Mbeya

Baadhi ya wafanyakazi wa TPSC wakifatilia mahafali hayo



No comments:

Post a Comment