Jana
tar. 13 Juni, 2018 Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa
Arusha imekutana na Ujumbe wa Idara ya Maadili & Nidhamu ya Chama
Tawala cha FRELIMO Kutoka Nchini Msumbiji.
Ujumbe huo uliongozwa na Katibu wa Sekretarieti ya Kamati Kuu na Gavana wa Jimbo la Mkoa wa Maputo Nchini Msumbiji Mh. Raimundo Maico Diomba Umekutana na Uongozi wa CCM Mkoa wa Arusha mapema jana Ofisi za CCM Mkoa wa Arusha ili kujifunza mambo kadha wa kadha ikiwemo ni jinsi gani CCM inaweza kusimamia na kuongoza Vikao vya ngazi mbalimbali kwa nyakati mbalimbali pindi kiongozi ama mwanachama anapokwenda kinyume na maadili ya Chama.
“Ama
kwa hakika tumejifunza mengi na kubadirishana mawazo jinsi ya
kuboresha Vyama vyetu viendelee kufanya vizuri kwa Wananchi wake ikiwemo
kusimamia vyema Maadili kwa wanachama na Viongozi wake
No comments:
Post a Comment