
Ngasa alilazimika kukopa fedha benki baada ya kuamriwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji kuilipa Simba Sh. milioni 45 alizochukua ili ajiunge nayo lakini akaikacha na kutua Yanga. Kamati hiyo pia ilimfungia mechi sita za awali za Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita kufuatia kesi yake hiyo dhidi ya Simba.
Hata hivyo, Yanga haikuwa tayari kutaja kiasi ambacho mchezaji huyo alikopa benki, alichokatwa na viongozi ambacho hakikupelekwa benki, wala kiasi cha deni kilichobaki.
Akizungumza jana jijini, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Jerry Muro, alisema kuwa tayari wamepokea maombi ya Ngasa lakini Yanga itatekeleza maombi hayo kwa masharti maalum.
Muro alisema kuwa ndani ya kipindi cha wiki moja Yanga itakuwa imelitatua suala la mshambuliaji huyo ili aweze kuitumikia vyema timu hiyo inayoongoza Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.
"Kulipa deni kuna taratibu zake, fedha za Yanga ni za wanachama na ni lazima utaratibu ufuatwe kabla ya kumlipia. Ngasa ameomba kulipiwa nasi tutamlipia kwa sababu bado tunamhitaji naye pia anatuhitaji," alisema Muro.
No comments:
Post a Comment