KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 2, 2015

SPIKA ATOA UFAFAFUNZI MUSWADA WA MNYIKA

images
Na Anitha Jonas-MAELEZO,Dodoma.
………………………………. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Anne Makinda ametoa ufafanuzi juu ya suala la Muswada binafsi wa Baraza la Vijana uliyowasilishwa na Mhe.John Mnyika Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) hapo mwaka jana. Mhe.Makinda alisema Ofisi yake inataratibu zinazofuatwa katika uwasilishwaji wa Miswada bungeni na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii ilifanya taratibu zake na kuiletea Ofisi yake taarifa ya makubaliano ya Muswada wa Serikali ndiyo utako somwa Bungeni baada ya kufuata taratibu zote muhimu. “Ofisi yangu haifanyi maamuzi binafsi katika uwasilishwaji wa Miswada Bungeni na zipo hatua mbalimbali Miswada inayopitia pamoja na Kanuni za Bunge zinatoa muongozo katika utekelezaji wake na Kamati huzingatia hayo na mwisho hutoa taarifa ya kuomba Muswada kusomwa ndani ya Bunge,”alisema Mhe.Makinda. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii Mhe.Said Mtanda (Mb) wa Mchinga CCM alisema Kamati ilipokea Miswada miwili ya kuundwa kwa Baraza la Vijana ukiwemo wa Mhe.John Mnyika Mb wa Ubungo CHADEMA na Muswada wa Serikali. Baada ya hapo Kamati ilikaa Kikao tarehe 20-31 Oktoba 2014 na kujadili Muswada huo ambapo pamoja na mambo mengine iliwaita wadau mbalimbali ambao walitoa maoni yao na mapendekezo ya Kamati,Kamati iliona Muswada huo haukuwa tayari na hivyo ulirudishwa katika Ofisi ya Spika tarehe 06 Novemba,2014. Aidha,Kamati ilipokea Muswada wa Serikali kuhusu hoja ya kuanzishwa kwa Baraza la Vijana Tanzania Muswada na Kamati ilipata nafasi ya kuujadili kwa kina,kupata maoni,ushauri na mapendekezo ya wadau na hivyo badae kamati iliamua kuwa mtoa hoja Binafsi na Serikali wakutane na na kushauriana kisha kupata muafaka wa Muswada upi uingie ndani ya bunge. “Kamati ilipata nafasi ya kujadili hoja zote mbili na kufanya uamuzi wa kidemokrasia wa mashauriano na maridhiano juu ya muswada upi uingie ndani ya Bunge.Aidha Kamati ilizingatia Kanuni ya 177 ya Kanuni za Kudumu za Bunge,inayosema akidi ya Mkutano wowote wa Kamati ya kudumu itakuwa theluthi moja ya wajumbe wote wa kamati,kwenye kikao hicho kulikuwa na wajumbe 13 kati ya 22 wa kamati nzima na hivyo theluthi moja ya wajumbe hao ni 7,wajumbe 9 walipiga kura ya Muswada wa Serikali usomwe bungeni wajumbe wanne wa walikataka Muswada binafsi uswomwe bungeni”,alisema Mhe.Mtanda. Mwisho Kamati ilikubali kwa pamoja mambo yote ya msingi yaliyomo kwenye Muswada binafsi yatumike kuboresha Muswada wa Serikali utakaowasilishwa Bungeni.

No comments:

Post a Comment