KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 25, 2016

WAFANYA BIASHARA KARIAKOO WACHANGIA MILIONI 60 WAHANGA WA TETEMEKO BUKOBA

5
NA HERIETH SEMGAZA
Wafanyabiashara katika soko la kariakoo lililopo jijini Dares salaam wameombwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kuwachangia wahanga wa tetemeko la Bukoba mkoani Kagera leo katika harambee iliyofanyika katikati ya soko la Kariakoo jijini Dar es salaam
Hayo yamesemwa na Philimin Romano Chonde Mwenyekiti wa wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo(JWK) ambapo alitaja jumla ya pesa na thamani ya vifaa mbalimbali vilivyochangwa  katika kampeni ya hiyo ,ambayo bado inaendelea amesema mpaka sasa wamepokea Jumla ya shilingi milioni 60 laki saba na mia Tano zimekuswanywa               Philimin Romano Chonde amesema  tunaendelea kupokea mchango wenu ili tuweze kuwasilisha kwa Waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa katika siku itakayopangwa, Aidha amewapongeza wanachama,wafanyabiashara wote waliojitokeza kutoa michango yao na kuwataka waendelee kujitoa katika shughuri mbalimbali za Kitaifa.
Nae SILVER MANDE mhazini Wa JWK amesema kuwa taasisi na wafanyabiashara wengine waendelee kujitokeza kwa wingi ili kutoa michango yao na kufanikisha kazi hiyo ambayo ni muhimu sana katika jamii yetu hasa kwa hawa wenzetu ambao walipata jamnga la Tetemeko la Ardhi huko Bukoba na kuathiri maisha yao na shughuli zao za kila siku.                  
Taasisi mbalimbali na wafanyabiashara tunaomba muwe mstari wa mbele kutoa michango na kwa yeyote atakaye kuwanacho alete ili tuweze kujumuisha rambirambi zetu na kuwasilisha kwa Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

No comments:

Post a Comment