KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 1, 2016

HATAREEE! LEO NI LEO UWANJA WA TAIFA SIMBA VS YANGA

Image result for SIMBA VS YANGA
Vigogo ambao pia ni mahasimu wa soka Tanzania bara kutoka mtaa wa kariakoo jijini Dar es salaam, Yanga na Simba,leo watapambana katika mechi ya kwanza  ya ligi kuu ya soka ya Tanzania bara a.k.a Ligi ya Vodacom itakayopigwa katika uwanja mkuu wa taifa jijini Dar es salaam. Timu hizo zilikuwa kambini kujiandaa kwa mechi hiyo ,Simba mpaka sasa ndio wanaongoza ligi baada ya kucheza Mechi 6 na wana pointi 16 wakifuatiwa na Stand United wenye Pointi 12 kwa Mechi 6. Nafasi ya tatu ni Yanga huku nafasi za nne na tano zipo Azam FC na Mtibwa Sugar zote zikiwa na pointi 10 kila mmoja.
Katika kuelekea mechi hiyo makocha wa timu hizo Joseph Omong wa simba na Hans van Pluijim, kila mmoja amesema kuwa timu itaibuka na ushindi.
Msimu uliopita, Yanga iliikung'uta Simba mabao 2-0 katika mechi zote mbili.

No comments:

Post a Comment