KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 15, 2017

MILIO YA RISASI YATANDA MJI MKUU WA IVORY COST

Wanajeshi waasi mjini Bouake, Mei 14, 2017
Ufyatulianaji mkali wa risasi umezuka katika miji miwili mikuu nchini Ivory Coast, wanajeshi wakiendelea kuasi kwa siku ya nne mtawalia.
Wanajeshi hao waliogoma wamefunga barabara nje ya kambi za jeshi katika mtaa wa kifahari Abidjan, mji mkuu wa kibiashara wa Ivory Coast, mwandishi wa BBC mjini humo anasema.
Wanajeshi watiifu kwa serikali wameelekea katika mji wa pili, Bouaké, ambapo ufyatulianaji wa risasi pia umesikika.
Mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Jenerali Sékou Touré ameapa kumaliza maasi hayo, ambayo yalitokana na mzozo kuhusu malipo.
Kupitia taarifa Jumapili, Jenerali Touré alisema wengi wa wamnajeshi hao waliogoma walikuwa awali wameitikia wito wa kuwataka wasitishe mgomo wao.
Lakini operesheni ya kijeshi imeanzishwa kwa sababu baadhi ya wanajeshi wameendelea kupuuza maagizo ya wakuu wao, amesema.
Wanajeshi hao waasi wameapa kujibu mashambulio iwapo watakabiliwa na wanajeshi watiifu kwa serikali.
Milio ya risasi imesikika katika kambi ya jeshi ya Akouédo, mtaa ambao huwa na wakazi wengi wa mapato ya wastani nchini Ivory Coast na ambapo pia raia wa kigeni hupenda sana kuishi, mwandishi wa BBC aliyepo Abidjan Tamasin Ford anasema.
Haki miliki ya picha AFP

No comments:

Post a Comment