KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 20, 2014

YANGA YALALA MORO,AZAM YASHINDA

Na Bin Zubeiry 

YANGA SC imeanza kwa kipigo cha mabao 2-0 Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kutoka Mtibwa Sugar, Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, mshambuliaji Genilson Santana ‘Jaja’ akikosa penalti.
 
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Dominick Nyamisana wa Dodoma, aliyesaidiwa na Ferdinand Chacha wa Mwanza na Milambo Tshikungu wa Mbeya, hadi mapumziko tayari Mtibwa Sugar walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0.

Bao hilo lilifungwa na mshambuliaji wa zamani wa Simba SC na DC Motema Pembe ya DRC, Mussa Hassan Mgosi dakika ya 16 aliyemalizia pasi ya kichwa ya Ame Ali na kumuwahi kipa Deo Munishi ‘Dida’ aliyetokea vizuri kutaka kudaka
Baada ya bao hilo, nyuki wakaingia uwanjani jambo lililosababisha wachezaji walale chini kwa dakika mbili, kabla ya wadudu hao kuondoka na mchezo kuendelea.

Almanusra Genilson Santana ‘Jaja’ aisawazishie Yanga SC dakika ya 32 baada ya kuunganisha vizuri kwa kichwa kona ya Haruna Niyonzima, lakini Hassan Ramadhani akauokoa ukiwa unaelekea nyavuni.

Dakika ya kwanza tu ya kipindi cha pili, Yanga SC walipata penalti baada Salim Mbonde kuunawa mpira kwenye eneo la hatari, lakini kipa Said Mohamed Kasarama akapangua kwa mguu mkwaju wa Jaja.

Dakika ya 47, Simon Msuva, aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Hamisi Kiiza ‘Diego’aliifungia Yanga SC bao, lakini refa akasema aliotea. Dakika ya 49 tena, Mrisho Ngassa alifunga bao lakini refa akasema aliotea pia.

Dakika ya 67, Simon Msuva alivamia langoni mwa Mtibwa na kutoa vitu vilivyokuwa chini upande wa nyavu kubwa na kukimbia navyo huku akikimbizwa na kipa Said Mohamed Kasarama kabla ya kuvitupa nje.

Dakika ya 82 mpishi wa bao la kwanza, Ame Ali aliifungia Mtibwa bao la pili baada ya kufanikiwa kuwahadaa mabeki wawili wa kati wa Yanga SC, Nadir Haroub ‘Cannaaro’ na Kevin Yondan kisha kumtungua Dida kufuatia pasi nzuri ya Hassan Ramadhani.

Yanga SC iliathiriwa na mabadiliko iliyoyafanya dakika za mwishoni kumtoa Mbuyu Twite aliyekuwa mhimili wa safu ya ulinzi na kuingiza mshambuliaji, Said Bahanuzi.

Kocha wa Yanga SC, Marcio Maximo ambaye alimfundisha kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime alipokuwa Taifa Stars alikuwa mnyonge baada ya meci hiyo. 

Kikosi cha Mtibwa Sugar kilikuwa; Said Mohammed, Hassan Ramadhani, David Luhende/Majaliwa Shaaban dk64, Salim Mbonde, Andrew Vincent, Shaaban Nditi, Ali Shomary, Muzamil Yassin, Ame Ali, Mussa Mgosi/Vincent Barnabas dk50 na Mussa Nampaka/Dickson Daud dk72. 

Yanga SC; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua/Omega Seme, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Mbuyu Twite/Said Bahanuzi dk72, Hassan Dilunga, Haruna Niyonzima, Genilson Santana ‘Jaja’, Mrisho Ngassa na Hamisi Kiiza/Simon Msuva dk46. 
Shujaa; Didier Kavumbangu akishangilia baada ya kuifungia Azam FC mabao mawili katika ushindi wa 3-1   

Beki Aggrey Morris akaipatia bao la pili Azam FC dakika ya 23 aliyemalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Kipre Tchetche kufuatia beki Gardiel Michael kuchezewa rafu na Bantu Admin.
Baada ya mabao hayo mawili ya haraka haraka, kocha wa Polisi Morogoro, Mohammed Adolph ‘Rishard’ alimpumzisha kiungo Bantu Admin na kumuingiza James Mganda.

 
Mabadiliko hayo kidogo yaliituliza Polisi na kuanza kufika kwenye lango la Azam, ingawa hawakufanikiwa kupata bao hadi dakika 45 za kwanza zilipokamilika. 
Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Danny Mrwanda alidhibitiwa vikali na mabeki wa Azam leo. 

  
Kipindi cha pili, Azam FC ilirudi vizuri na kusukuma mashambulizi mfululizo langoni mwa Polisi, lakini mshambuliaji Kipre Tchetche alikosa mabao matatu ya wazi.

 
Nahoda Bakari aliipatia bao Polisi dakika ya 60 baada ya kuanzishiwa kona fupi na kumtungua kwa shuti la umbali 22 kipa Aishi Manula.

 
Didier Kavumbangu aliifungia bao la tatu Azam FC dakika ya 90 akimalizia krosi ya Farid Malik.

 
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, David Mwantika, Aggrey Morris, Kipre Balou, Himid Mao/Khamis Mcha ‘Vialli’ dk72, Mudathir Yahya, Didier Kavumbangu, Kipre Tchetche/Farid Malik dk72 na Salum Abubakar.

 
Polisi Moro; Tony Kavishe, Rogeri Fred, Simon Fanuel, Ally Feruzi Telu, Lulanga Mapunda, Said Jella, Bantu Admin/James Mganda dk22, Nahoda Bakari/Suleiman Kassim ‘Selembe’ dk65, Danny Mrwanda, Machaku Salum na Nicholas Kabipe/Edgar Charles dk65.

              


    

No comments:

Post a Comment