Kamishna
Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(suti nyeusi), akiwa amesimama
wakati mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la
Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila,
ulipowasili tayari kwa kuuagwa rasmi nyumbani kwake Ukonga, Dar es
Salaam jana Oktoba 20, 2014. Wa kwanza kushoto ni Kamishna Mkuu Mstaafu
wa Magereza, Nicas Banzi, wa pili kushoto ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa
Magereza, Jumanne Mangara, wa kwanza kulia ni Kamishna wa Fedha na
Utawala, Gaston Sanga, wa pili kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji
wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja, akisaini katika kitabu
cha Maombolezo nyumbani kwa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa
Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen
Nzawila ambaye amefariki Jumapili tarehe 19 Oktoba, 2014 katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam.
Mchungaji
wa Kanisa la Moravian, lililopo Ukonga Banana Relini, Hansi Mwakijoja,
akiwaongoza waombolezaji kwa sala kabla ya kuuaga rasmi mwili wa
aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja, akitoa heshima za
mwisho kwa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza.
Baadhi
ya Maofisa na Askari wa Jeshi la Magereza, wakiwa wamejipanga katika
mstari tayari kuuaga mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa
Jeshi la Magereza jana Oktoba 20, 2014 Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa leo kuelekea Tutuo Wilayani
Sikonge, Mkoani Tabora kwa Mazishi.
Mke
wa Aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, akiwa na
majonzi makubwa na waombolezaji kabla ya kuuaga rasmi mwili wa mume
wake.
Sehemu
ya Waombolezaji waliojitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu
Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, wakisikiliza kwa makini wasifu wa
Marehemu kabla ya kuuaga rasmi.
Bendi
ya Jeshi la Magereza, ikitumbuiza katika hafla fupi ya kuuaga mwili wa
aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila.
Mwili
wa aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkuu Msaidizi wa Jeshi la Magereza,
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stephen Nzawila ukiwa umebebwa
na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kabla ya kuagwa rasmi leo
Oktoba 20, 2014 nyumbani kwake, Ukonga Dar es Salaam.
(Picha na Lucas Mboje, wa Jeshi la Magereza).
(Picha na Lucas Mboje, wa Jeshi la Magereza).
No comments:
Post a Comment