Mhe. Liberata Mulamula, Balozi wa Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania nchini Marekani amemkaribisha Mhe. Ammon Mutembwa, Balozi mpya
wa Jamhuri ya Zimbabwe Ubalozini Tanzania House, Washington DC,
Marekani, Jumatano Novemba 26, 2014. Katika mazungumzo yake na Balozi
Mutembwa, Mhe. Balozi Mulamula alimweleza Balozi huyo kwamba ajisikie
kwamba yuko nyumbani. Mhe. Mulamula aliendelea kwa kusema kwamba
Tanzania na Zimbabwe zina mahusiano ya kihistoria na kwa msingi huo ni
vyema kutafsiri kwa vitendo mahusiano hayo kwa kujenga mashirikano zaidi
baina yao. Mhe. Mulamula alifurahishwa na ziara hiyo ya Balozi Mutembwa
Ubalozini na kuahidi kwamba kupitia kwa Jumuia ya Ushirikiano wa Nchini
za Kusini mwa Afrika (SADC), Tanzania na Zimbabwe zina fursa ya kutosha
kuziwakilisha nchi zao nchini Marekani kwa manufaa ya Serikali na
wananchi wao. Kwa upande wake, Mhe. Balozi Mutembwa alimshukuru Mhe.
Balozi Mulamula kwa kumkaribisha Ubalozini na kwamba kwa vile ndio
kwanza ameripoti katika kituo chake kipya cha kazi atashukuru sana
kupata mwongozo wake na ushauri kutoka kwake ili aweze kutekeleza
majukumu yake ya kiuwakilishi nchini Marekani kwa ufanisi. Balozi
Mutembwa alisema pia kwamba moja ya jukumu lake kubwa ni kuhakikisha
vikwazo ilivyoekewa nchi yake na Marekani vinaondolewa kupitia
mazungumzo na kujenga maelewano mazuri baina ya nchi yake na Marekani. Mhe.
Liberata Mulamula, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Marekani na Mexico(Kulia) akimkaribisha Mhe. Ammon Mutembwa,(Kushoto).
Balozi Mpya wa Jamhuri ya Zimbabwe nchini Marekani Ubalozini Tanzania
House Washington DC,Marekani. Mhe.Balozi Mulamula na Mhe. Balozi Mutembwa katika picha ya kumbukumbu baada ya kusaini kitabu cha wageni. Mhe.
Balozi Liberata Mulamula(Katikati) akiwa katika mazungumzo na mgeni
wake Mhe.Balozi Ammon Mutembwa (Wa pili kushoto) huku Maofisa wao Bw.
Suleiman Saleh (Wa kwanza kulia) na Bw. Whatmore Goora (Wa kwanza
kushoto) wakifuatilia. Picha na Mugendi Zoka
No comments:
Post a Comment